logo

NOW ON AIR

Listen in Live

7 wafariki katika maporomoko ya ardhi Gilgil

Polisi wlisema maporomoko hayo yalisomba kijiji na kung'oa nyumba katika mkondo wake.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri28 March 2023 - 10:49

Muhtasari


• Mashirika ya kutoa misaada yakiongozwa na shirika Msalaba mwekundu yameanzisha shughuli ya kuwasaidia waathiriwa.

HELL'S GATE : Polisi wakiwa wamebeba moja ya miili iliyoopolewa kwenye korongo katika Hifadhi ya Taifa ya Hell's Gate, ambapo watu saba walikufa maji waliposombwa na mafuriko. Picha: FILE

Mvua kubwa inayoendelea kunyesha katika maeneo mbali mbali nchini imeendelea kusababisha maafa huku watu saba wakiaga dunia kutokana na maporomoko ya ardhi katika eneo la Gilgil.  

Saba hao wanawake watatu na watoto wanne walifariki baada ya kusombwa na tope kutoka kwa vilima vya Eburru Mbaruku katika kijiji cha Ol Jorai huko Eburru Mbaruk, Kaunti Ndogo ya Gilgil jana usiku. 

Akithibitisha kisa hicho, OCPD wa Gilgil Francis Tumbo alisema kuwa maporomoko hayo ya udongo yalisomba kijiji na kung'oa nyumba na majengo yaliyokuwa katika mkondo wake na hivyo kusababisha vifo vya watoto wanne na watu wazima watatu. 

Mashirika ya kutoa misaada yakiongozwa na shirika Msalaba mwekundu yameanzisha shughuli ya kuwasaidia waathiriwa.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved