logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Athari za uraibu wa mtu kujimalizia hisia za mapenzi

Mraibu hujitomasa sehemu zake za siri mwenyewe ili kujisisimua kimapenzi.

image
na

Yanayojiri18 September 2023 - 11:09

Muhtasari


•Wengi wa wanarika hupatwa na msongo wa mawazo kutokana na athari za kujichua

punyeto yaharibu ndoa nyingi za vijana

Uraibu wa wanawake au wanaume kujimalizia hisia zao za kimapenzi ni tatizo ambalo linazidi kukithiri katika jamii na tushia ndoa nyingi miongoni mwa wanajamii.

Hiki ni kitendo cha mtu kutomasa sehemu zake za siri mwenyewe ili kujisisimua kimapenzi.

Kitendo hiki kulingana na wataalam ni cha kawaida lakini kikifanywa muda mrefu huathiri uwezo wa muhusika kutekeleza majukumu yake ya chumbani hasa kwa wanaume ikiwa ameoa. 

Kupotea kwa nguvu za kiume: kuligana na washauri wa maswala ya ndoa  ni wazi kuwa wengi wa vijana ambao ni waraibu wa kitendo hiki huchagia sana mtu kupoteza uwezo wa mwanamume kumridhisha mpenziwe kwa sababu kutumia mikono yao kujichua huathiri mishipa ya fahamu inayoenda kwenye uume.

Utasa wa muda kwa wanaume: Mazoea haya pia hupunguza sana kiasi cha manii kinachopatikana kwenye korodani hali inayopunguza uwezo wa mwanamume kumtunga mwanamke mimba.

Jambo hili la kukosa watoto ndani ya familia husababisha hali aa swintofahamu katika ndoa na kuchangia msongo wa mawazo miongoni mwa vijana.

Washauri wa maswala ya ndoa wanaonya kuwa mazoea ya kujichua pia mara nyingi huharibu uhusiano kati ya wapenzi kwani kila mmoja hana hamu na mwenzake kwa sababu kila anapokuwa na hisia za kimwili anajitimizia hali ambayo ikiendelea kwa muda husambaratisha ndoa.

Kushidwa kufikisha mwenzako kileleni: Waraibu wengi wa kujichua  hasa wanaume hushindwa kuhimili tendo la ndoa kwa wakati ufaao na kumaliza safari mapema kabla ya ndege ya wenzao kutua uwanjani.   

 

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved