logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Bei ya petroli huenda ikapanda hadi Sh300- Waziri Chirchir

Kwa sasa bei ya petroli inauzwa kwa Sh217 jijini Nairobi.

image
na

Yanayojiri06 November 2023 - 10:18

Muhtasari


•Kupanda kwa bei ya mafuta kwa upande wake kutasababisha kupanda kwa bei za bidhaa nyingine, hatua iliyoibua kejeli mbalimbali kutoka kwa wananchi waliolalamikia ughali wa maisha.

Mhudumu akiweka gari Mafuta

Waziri wa Nishati Davis Chirchir amesema kuwa  huenda bei ya mafuta ya super petroli ikaongezeka hadi  kufikia shillingi  mia tatu ikiwa bei ya kimataifa itaongezeka.

"Bei za kimataifa za mafuta zinaweza kupanda hadi dola 150,Hii inamaanisha kuwa bei zetu za petroli zinaweza kupanda hadi Sh300 kwa lita kwenye Bomba,Tunatumai haitafika huko," alisema.

Waziri huyo alisema hayo  alipokuwa  akizungumza  mbele ya kamati ya Mazungumzo ya Kitaifa  Bomas of Kenya Jumatatu.

Katikati mwa mwezi Oktoba, Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Petroli nchini Kenya ilitangaza  bei mpya ya mafuta hadi rekodi ya juu katika historia ya nchi, lita moja ya petroli sasa ikiuzwa kwa Sh217.

Kupanda kwa bei ya mafuta kwa upande wake kutasababisha kupanda kwa bei za bidhaa zingine, hatua iliyoibua kejeli mbalimbali kutoka kwa wananchi waliolalamikia ughali wa maisha.

Kenya na Afrika Kusini zimekuwa zikikabiliwa na ongezeko la gharama ambalo limechangiwa na tatizo la ongezeko la mafuta duniani.

Kulingana na Mtazamo wa hivi karibuni wa Masoko ya Bidhaa  mzozo wa Israel na Gaza umechangia pakubwa  katika bei ya bidhaa  kupanda kutokana na kukatika kwa mzunguko wa kimataifa wa usambazaji bidhaa.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved