logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Idara ya utabiri wa anga yaonya kuhusu mvua nyingi katika siku mbili

Idara hiyo imewataka wakaazi wa maeneo hatari kuchukua tahadhari ya mapema

image
na Brandon Asiema

Yanayojiri14 November 2024 - 08:39

Muhtasari


  • Wakenya wameshauriwa kutoendesha gari ama kutembea kwenye sehemu zilizofunikwa na maji. Ushauri ya kutojikinga mvua chini ya miti umetolewa ili kueouka visa vya kupigwa na radi.
  • Wakaazi wa maeneo ambayo yanajulikana kushuhudia maporomoko ya ardhi haswa kwenye miteremko ya Aberdare na Mlima Kenya wametakiwa kuwa waangalifu.

caption

Idara ya utabiri wa haliya anga ya Kenya imetahadharisha kuhusu mvua nyingi inayotarajiwa kunyesha kati ya Alhamisi Novemba 14 na Ijumma Novemba 15 katika baadhi ya maeneo nchini.


Kupitia ujumbe kwa vyombo vya habari idara hiyo imetahadharisha kuwa mvua ya Zaidi ya milimita 20 chini ya masaa 24 huenda ikanyesha kwenye baadhi ya sehemu ikiwemo maeneo ya kati ya bonde la ufa, nyanda za chini za kusini mashariki na maeneo ya kati mwa taifa ikiwemo Nairobi.


Idara hiyo imewataka Wakenya katika sehemu ambazo zitaathirika kuchukua tahadhari ya mapema kwani majihuenda yakawa mengi na kusababisha mafuriko.


Maeneo ya Tharaka Nithi, Nyeri, Kimbu, Meru, Embu, Kirinyaga, Bomet, Kericho, Nakuru, Isiolo, Nyandarua, Laikipia, Machakos, Kitui, Narok ,Kajiado na Murang’a zinatarajiwa kuathirika na mvua hiyo ya siku mbili.


Vile vile, idara hiyo imesema kuwa mvua hiyo inatarajiwa kuongezeka hata zaidi siku ya Ijumaa katika sehemu za nyanda za chini za kusini mashariki mwa nchi,maeneo ya kati ya nchi ikiwemo Nairobi kufikia viwango vya milimita.


Kwenye tahadhari ya idara ya hali anga, Wakenya wameshauriwa kutoendesha gari ama kutembea kwenye sehemu zilizofunikwa na maji. Ushauri ya kutojikinga mvua chini ya miti umetolewa ili kueouka visa vya kupigwa na radi.


Vile vile, wakaazi wa maeneo ambayo yanajulikana kushuhudia maporomoko ya ardhi haswa kwenye miteremko ya Aberdare na Mlima Kenya wametakiwa kuwa waangalifu.



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved