logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Washukiwa 2 wanaswa na kokeni na bangi jijini Nairobi

Washukiwa wanazuiliwa katika kituo cha polisi wakisubiri kufikishwa mahakamani

image
na Brandon Asiema

Yanayojiri26 November 2024 - 10:14

Muhtasari


  • Vidonge tisa vya kokeni na misokotokadhaa ya bangi ilipatikana kwenye gari la washukiwa hao waliokamatwa.
  • Mihadarati hiyo inakisiwa kugharimu shilingi laki tano na elfu nne, gramu moja ya kokeni ikiuzwa kwa shilingi elfu mbili na mia nane.


Maafisa wa polisi kutoka kitengo cha Operation Support Unit cha DCI, wanawazuilia washukiwa wawili wa ulanguzi wa dawa za kulevywa waliokamatwa katika eneo la Ruiru.

Washukiwa hao waliokuwa katika kituo kituo kimoja cha petrol eneo hilo , walikamatwa na gramu 180 ya kokeni pamoja na misokoto kadhaa ya bangi inayodaiwa ilikuwa inangoja mnunuzi.

Kulingana na taarifa ya DCI, wawili hao wamekuwa wakitafutwa na polisi kwa kuhusika na ulanguzi wa mihadarati jijini Nairobi na sehemu kadhaa za kaunti ya Kiambu  kwa muda mrefu na baada ya mawindo ya saa kadhaa, polisi walifanikiwa kuwakamata wawili hao hatimaye.

Katika msako wa polisi kwenye gari lililokuwa limeegeshwa na washukiwa hao, vidonge tisa vya kokeni vyenye thamani ya shilingi 504,000 zilipatikana kwenye gari lao pamoja na misokoto kadhaa ya bangi. Taarifa ya polisi imebaini kuwa washukiwa hao walikuwa wanauza gramu moja ya kokeni kwa shilingi 2,800.

Washukiwa hao wanazuiliwa katika kituokimoja cha polisi jijini Nairobi wakisubiri kufikishwa mahakamani kujibu mashtaka ya ulanguzi wa mihadarati. Aidha polisi wanawatafuta washukiwa wengine ambao wametambuliwa kuhusika na ulanguzi wa mihadarati.



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved