logo

NOW ON AIR

Listen in Live

NTSA yaahidi kuchukua hatua dhidi ya uendeshaji mbovu wa PSV uliorekodiwa

Kwenye magari hayo, abiria walionekana wakiwa wametoa vichwa nje wengine wakiwa wamekalia kwenye madirisha ya magari hayo licha ya mwendo wa kasi uluokuwa unaendeshwa

image
na Brandon Asiema

Yanayojiri23 December 2024 - 11:46

Muhtasari


  • NTSA imeendesha msako wa kuangalia vidhibiti mwendo kwenye magari katika barabara kuu nchini ikiwemo Kakamega - Kisumu katika eneo la Iguhu.
  • NTSA imesema kwamba kitendo hicho kilichorekodiwa ni kinyume cha sheria ambacho hakukubaliki na tayari wamiliki wa magari hayo ya PSV wametakiwa kufika mbele ya mamlaka hiyo.


Mamlaka ya uchukuzi na usalama barabarani NTSA imeahidi kuwachukulia hatua za kisheria wamiliki wa magari ya utumishi wa umma ambayo yalionekana kwenye kanda ya video iliyorekodiwa yakiendeshwa kwa namna isiyostahili katika barabara moja.

Katika video iliyochapishwa kwenye mtandao wa X, na shirika moja lisilo la kiserikali  lenye malengo ya kuhamisisha madereva na makanga kuzingatia usalama barabarani mnamo Jumatatu asubuhi Disemba 23, magari mawili ya kuwabeba abiria 14 yaliyoenekana yakiendeshwa kwa mkondo wa wimbi kwenye barabara yenye kona.

Kwenye magari hayo, abiria walionekana wakiwa wametoa vichwa nje wengine wakiwa wamekalia kwenye madirisha ya magari hayo licha ya mwendo wa kasi uluokuwa unaendeshwa kwenye magari yenyewe.

NTSA imesema kwamba kitendo hicho kilichorekodiwa ni kinyume cha sheria ambacho hakukubaliki na tayari wamiliki wa magari hayo ya PSV wametakiwa kufika mbele ya mamlaka hiyo.

“Hili halikubaliki. Wamiliki wa magari hayo wameitwa. Tutachukua hatua.”  NTSA ilisema kwa ujumbe wake kwenye mtandao wa X.

Hayo yakijiri, mamlaka hiyo ya NTSA imeendesha msako wa magari yasiyokubalika barabarani katika sehemu tofauti tofauti nchini ilikuimarisha usalama barabarani.



Mnamo Jumatatu, maafisa wa NTSA walifanya msako katika barabara ya Kakamega – Kisumu kwenye eneo la Iguhu ambapo takribani watu 13 walipoteza maisha baada ya trela kusafirisha mizigo kupoteza mweleko na kungoga magari mawili wa abiria.

Vile vile msako ulifanywa katika kaunti ya Nyamira maafisa wakichunguza vidhibiti mwendo kwenye magari kwa mujibu wa agizo lililotolewa na mkuu wa mawaziri Musalia Mudavadi.



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved