logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mbunge wa Nyali Mohamed Ali afanyiwa upasuaji wa goti

Mbunge huyo alipata jeraha wakati wa michezo ya wabunge wa mataifa ya jumuiya ya Afrika Mashariki

image
na Brandon Asiema

Yanayojiri27 December 2024 - 17:12

Muhtasari


  • Mbunge huyo ametangaza kuwa amesimamisha ratiba yake yote ya kisiasa wakati wa kuuguza majeraha


Aliyekuwa mwanahabari mpekuzi na sasa ni mbunge wa eneo bunge la Nyali Mohamed Ali maarufu kama Jicho Pevu, ameweka wazi kwamba amefanyiwa upasuaji wa goti kutokana na jeraha alilolipata katika michezo iliyowaleta pamoja wabunge wa mataiafa ya jumuiya ya Afrika Mashariki.

Mashindano hayo yalifanyika jijini Mombasa kwa takribani wiki mbili ambapo michezo mbali mbali ikiwemo soka, riadha, mpira wa vikapu na mchezo wa kuvuta kamba.

Kupitia ujumbe kwa anwani yake ya mtandao wa Instagram ,bunge huyo amesema kwamba upasuaji uliofanywa kwenye goti lake ulifanyika kwa mafanikio ila daktari wake alimweleza kuwa atapunguza kutembea kwa miezi mitatu ili apatge nafuu kamili.

Mbunge huyo ametangaza kuwa amesimamisha ratiba yake yote ya kisiasa wakati wa kuuguza majeraha ila amehakikishia wakaazi wa eneo bunge la Nyali kuwa shughu;li za ofisi yake zitafanyika bila kuhitilafiwa.

“Nina furaha kuwajulisha kuwa nimefanyiwa upasuaji wa goti vyema ila daktari wangu ameniambia nipunguze matembezi kwa angalau miezi mitatu  kuhusu uponyaji kikamilifu.” Aliandika mbunge huyo kwenye ukurasa wake wa Instagram.

Jicho Pevu hata hivyo amewataka wananchi kumkumnbuka katika maombi yao anapoendelea kupata nafuu akiahidi kuwa atarejea tena akiwa na nguvu zaidi.



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved