logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Tume ya kutetea haki ya kibinadamu nchini Kenya yataka baadhi ya viongozi kujiuzulu

Baadhi ya viongozi wamemulikwa na tume ya kutetea haki za kibinadamu kutokana na matamshi yao kuhusu visa vya utekaji nyara.

image
na OTIENO TONNY

Yanayojiri07 January 2025 - 14:37

Muhtasari


  • Hii inajiri baada ya baadhi  ya vijana waliotekwa nyara kuachiliwa.
  • Wakati huo , KHRC inamtaka inspekta jenerali wa polisi Douglas Kanja kuwasilisha ombi la kujiuzulu kutokana  utekaji nyara  chini ya ulinzi wake.



Msururu ya utekaji nyara ukiendelea kushuhudiwa nchini, chama kinachotetea haki ya kibinadamu{KHRC}  kimewasuta baadhi ya viongozi serikalini kikiwataka kujiuzulu kutokana na matamshi yao yanayodhaniwa kutojali utekaji nyara ambao umesuhudiwa nchini tangu maandamano ya vijana ya mwezi wa sita mwka uliopta.

Shinikizo hili linajiri baada ya baadhi  ya vijana waliotekwa nyara kuachiliwa. KLHRC ilitaja baadhi ya majina ya viongozi ambao waliwataka kujiuzulu kutokana na matamshi waliotoa wakati taifa lilikumbwa na wimbi la utekaji nyara kwa  vijana.

Baadhi ya majina ya viongozi waliotajwa na tume hiyo ni pamoja na naibu rais Kithure Kindiki, waziri wa mambo ya ndani Kipchumba Murkomen, kiongozi wa wengi katika bunge la kitaifa Kimani Ichung'wah, spika wa seneti Amason Kingi, mbunge wa Kapseret Oscar Sudi, mbunge wa Sirisia John Waluke na mbunge wa Tiaty William Kamket kuhusu matamshi yao katika wakati tete ambapo Wakenya wanatafuta majibu juu ya utekaji nyara unaotekelezwa.

Wakati huo, KHRC inamtaka inspekta jenerali wa polisi, Douglas Kanja kuwasilisha ombi la kujiuzulu baada ya utekaji nyara huo kutokea chini ya ulinzi wake.

Kulingana na tume hiyo, maoni yanayotolewa na wanasiasa hao yanakiuka utawala wa sheria na nyadhifa za uongozi wanazoshikilia.

Tume hiyo inayotetea haki za kibinadamu inataka uchunguzi usio na upendeleo na wa kina kufanywa kuhusu kauli wanazozitoa kuhusiana na visa vya vijana wanaowajibisha serikali kutekwa nyara.

KHRC imeshauri kuwa viongozi watakaopatikana na hatia wawajibishwe kwenye asasi husika pamoja na kuzuiwa kushikilia nyadhfa za umma. .


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved