logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Wakaazi wenye hasira waacha maiti nyumbani kwa mshukiwa wa mauaji

Wanaume wawili wanashukiwa kuhusika katika mauti ya marehemu mwenye umri wa miaka 16

image
na Brandon Asiema

Yanayojiri08 January 2025 - 16:27

Muhtasari


  • Mwili wa marehemu ulipatikana asubuhi ya Disemba 25 karibu na mto Thiba katika kaunti ndogo ya Mwea Magharibi.
  • Wakaazi wanataka familia ya washukiwa kufurushwa kutoka kijijini hapo.


Wakaazi wenye hasira na ghadhabu waliamua kuchukua sheria mkononi kwa kuupelekwa mwili wa msichana anayedaiwa kuuliwa kwenye boma la mshukiwa wa mauaji ya marehemu na kkuacha mlangoni pa mshukiwa huyo.

Kisa hicho cha Jumatano mchana kilishudia wakaazi wenye hasira wakishambulia maboma mawili ya washukiwa katika eneo la Mahigaini na Gushue katika kaunti ndogo ya Mwea Mashariki.

Kwa mujibu wa taarifa, mwili wa msichana huyo mwenye umri wa miaka 16 ulipatikana asubuhi ya Krisimasi karibu na mto Thiba katika kaunti ndogo jirani ya Mwea Magharibi.

Katika kisa hicho, polisi walilazimika kutumia vitoa machozi kusambaratisha umma uliokuwa na hasira walipopelekwa mwili wa msichana huyo ukiwa jenezani kwenye boma la mshukiwa mmoja.

Ghadhabu za wanakijiji zilielekezwa kwa familia ya mshukiwa huyo zikiitaka mamlaka kuhakikisha familia ya mshukiwa inafurushwa kutoka kwa kijiji hicho. Wanakijiji wanadai kuwa jamaa wa familia hiyo alihusika katika mauti ya marehemu.

”Hii familia pia kama watu wa hii kijiji mnaomba tutafanya hivi si mnataka haki.”

“Familia ya mwenye amefanya hii kitendo wote wahame.”

Sauti za wakaazi wenye hasira walisikika wakilalama


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved