logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mshtuko huku Askofu akipatikana akishiriki mapenzi na bintiye Homabay

Askofu mmoja katika county ya Homabay amewashangaza wenyeji baada ya kufumaniwa akiwa kwenye mapenzi na mwanawe.

image
na Japheth Nyongesa

Yanayojiri16 January 2025 - 12:01

Muhtasari


  • Askofu alifumaniwa na mwanakijiji mmoja akiwa katika tendo na mwanawe ambaye ni mama wa watoto watatu.
  •  Askofu amekamatwa akiwa nyumbani kwake pamoja na mwanawe.


Askofu mmoja katika kaunti ya Homabay amewashangaza wenyeji baada ya kufumaniwa akishiriki mapenzi na bintiye..

Maafisa wa usalama kutoka kaunti ndogo ya Rangwe wanamzuilia mwanaume huyo kwa kosa la kuhusika kwenye mapenzi na mwanawe wa damu.

 Maafisa walipata habari kutoka kwa maafisa wenzao wa kituo cha Ndiru baada ya kupashwa habari na wanakijiji.

Kulingana na walioshuhudia, askofu alifumaniwa na mwanakijiji mmoja akiwa katika tendo na mwanawe ambaye ni mama wa watoto watatu.

Msimamizi wa kituo cha polisi cha Rangwe  Magdaline Chebet alisema kwamba walipata habari kutoka kwa wanakijiji walioshangazwa na tabia za mmoja wao baada ya kumfumania akiwa kwenye tendo la ndoa na mwanawe ambaye alikuwa ameaoleka hapo awali na baadaye wakatengana na aliyekuwa mumewe.

Shinkizo za wanakijiji ziliwafanya maafisa wa polisi wa kituo hicho cha Ndiru, wakiongozwa na mkubwa wa kituo hicho kumtafuta mshukiwa na kumkamata.

Askofu alikamatwa nyumbani kwake pamoja na mwanawe.

Kwa sasa mshukiwa amezuiliwa katika kituo cha polisi cha Ndiru huku uchunguzi zaidi ukiendelezwa na maafisa wa usalama

Bintiye askofu, alipelekwa hospitalini, baadaye akahojiwa na kuachiliwa kurudi nyumbani.



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved