logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Raila Odinga afanyiwa maombi maalum kabla ya uchaguzi wa AUC

Ni maombi ambayo yaliandaliwa katika ukumbi wa Bomas yakiongozwa na akina mama

image
na Evans Omoto

Yanayojiri10 February 2025 - 16:25

Muhtasari


  • Vilevile katika maelezo ya Odinga aliashiria pakubwa kuwa analifahamu vyema bara la Afrika na matatizo yanayolikumba 
  • Kulingana na hotuba yake Raila Odinga alionyesha matumaini makubwa ya kuchaguliwa akisema kuwa  alikuwa amefanya kampeni ya kutosha 

Raila Odinga afanyiwa maombi  maalum kabla ya uchaguzi wa AUC

Ni maombi ambayo yaliandaliwa katika ukumbi wa Bomas yakiongozwa na akina mama kusudio likiwa ni kumwombea Odinga. Bwana Odinga ambaye aliandamana na mkewe bi Ida Odinga alionekana mpwamu na mwenye furaha wakati wa hafla hiyo.

Kulingana na hotuba yake Raila Odinga alionyesha matumaini makubwa ya kuchaguliwa akisema kuwa  alikuwa amefanya kampeni ya kutosha na kuzuru mataifa yote ya Afrika ambapo alikutana na viongozi mbalimbali wa nchi tofauti waliomhakikishia kumpigia kura.

Odinga aliwaonea wanawake Fahari huku akimshukuru mkewe kwa kumjali pakubwa, Odinga alisema kuwa alikuwa na mkutano wa dharura ambao alisitahili kushiriki lakini ukahairishwa akirejelea usemi kuwa mama Ida Odinga alimkumbusha kuwa siku hiyo likuwa imetengwa kwa ajili yake .

 Kulingana na mujibu wa maelezo ya Odinga  alikuwa na Imani isiyotetereka na hakikisho kuwa angeibuka mshindi alieleza historia fupi ya kulinganisha mwaka wa huu wa 2025 na ule wa 2005 akisema kuwa uasisi na upatikaji wa Katiba mpya na  chama chake cha ODM ulifanyika katika ukumbi huo wa Bomas hivo akawa anakumbuka siku hiyo kama siku ambayo itazaa matunda .

Vilevile katika maelezo ya Odinga aliashiria pakubwa kuwa analifahamu vyema bara la Afrika na matatizo yanayolikumba akisema kuwa matatizo yalio hapa nchini Kenya ni sawa na matatizo ambayo yaliokuwa yakizikumba nchi nyingi za afrika kama elimu,miundomsingi bora na mshikamano wa nchi za Afrika kwa jumla.

Raila alishauri akisema kuwa mapenzi yake ni kuona mataifa yote yakifikia kilele cha ufanisi kwanzia nyumbani hadi sehemu nyingine za ulimwengu aidha alionekana kumbariki gavana wa Nairobi bwana Johnson Sakaja akimwita kijana wake usemi ambao ulifasiriwa kama njia ya kumbarki bwana Sakaja na kumtakia kila la heri katika safari ya kutafuta ugavana kwa awamu ya pili iwapo itawadia.

Zimesalia siku nne kabla ya uchaguzi huo kutimia ambapo iwapo Odinga atachaguliwa bila shaka masikani yake yatakuwa nchi ya Uhabeshi Addisababa kama taifa la Kenya tunasema kila la heri kwake Raila Mungu amkirimie baraka za ushindi.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved