logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Rais Ruto akutana na mabalozi katika Ikulu ya Nairobi

Ajenda ya mkutano huo ililenga kuzungumzia hali ya machafuko nchini DRC.

image
na Evans Omoto

Yanayojiri10 February 2025 - 15:05

Muhtasari


  • Ruto mapema leo Jumatatu alikutana na wawakilishi wa mashirika mbalimbali ya nchi za kigeni wakiwemo mabalozi wa mataifa ya nchi za kigeni katika ikulu kuu ya Nairobi.
  • Ruto alisisitiza kuwepo kwa umoja kati ya mataifa ya wanachama wote akikariri kuwa amani katika nchi ya DRC haitaletwa kwa kutumia nguvu za jeshi bali kwa mazungumzo.

Ruto akutana na mabalozi katika Ikulu ya Naiobi

Rais Wiilliam Ruto mapema leo Jumatatu alikutana na wawakilishi wa mashirika mbalimbali ya nchi za kigeni wakiwemo mabalozi wa mataifa ya nchi za kigeni katika Ikulu kuu ya Nairobi.

Ajenda ya mkutano huo ililenga kuzungumzia hali ya machafuko nchini DRC ambako kumekuwa na hali ya utovu wa usalama katika taifa hilo.

Katika mkutano huo, rais Ruto alisistiza kuwepo kwa mazungumzo ya upatanishi kama njia ya kipekee ya kuleta amani katika taifa la Kongo ambalo ni mwanachama wa muungano wa  jumuiya ya mataifa ya afrika mashariki EAC na SADC.

Itakumbukwa vyema katika kikao kilichowaleta wanachama wote wa SADC katika mkutano ambao ulifanyika  Dodoma Tanzania ambapo rais Amason Nangabo  wa Zimbabwe ambaye ndiye mwenyekiti wa SADC ili kuzungumzia hali tete ya usalama DRC.

Mkutano huo ulipofanyika rais William Ruto alisisitiza kuwepo kwa umoja kati ya mataifa ya wanachama wote akikariri kuwa amani katika nchi ya DRC haitaletwa kwa kutumia nguvu za jeshi bali kwa mazungumzo na mapatano ya amani.

Taifa la DRC limekuwa likiisuta nchi ya Rwanda kwa madai ya kutuma wanajeshi wake katika ukanda wa Kivu ulio kasikazini ya Kongo wakishirikiana na kuundi la M23 ili kuuteka mji huo na kusababisha maafa na mahangaiko ya wananchi jambo ambalo Rwanda  kupitia kwa rais Paul Kagame alipinga vikali.

Rais Ruto alipokuwa akihutubia umma uliojaa viongozi na wawakilishi mbalimbali aligusisa pia suala la kuwa na hali nzuri ya mazingira ya tabianchi akinadi kuwa utunzaji wa mazingira ni jambo la manufaa sana kwa nchi yoyote ile.

Kiongozi wa nchi vilevile alizungumzia ushirikiano na umoja wa mashirika ya nchi mbalimbali katika viwango mbalimbali akirejelea makubaliano na mikataba mbalimbali ambayo inalenga kujenga ukuruba na wepesi wa kufanya biashara bila vikwazo vyovyote.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved