logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Ruto aungwa mkono na Marais wengine akitaka mabadiliko katika mifumo ya mikopo kwa Afrika

Rais Ruto aliungwaa mkono na marais wa afrika alipokuwa akihutubia kongamano la Pamoja la 38 la marais wa Afrika mjini Addis Ababa Ethiopia.

image
na Evans Omoto

Yanayojiri14 February 2025 - 15:02

Muhtasari


  • Ruto alisema kuwa kuwa mfumo wa sasa umekuwa ukinyanyasa baadhi ya mataifa ya afrika na kueneza ubaguzi kwa mataifa mengine
  •  Utafiti unaashria kuwa bara la Afrika lina uwezo wa kujisimamia kiuchumi na kimaendeleo.

Rais Ruto aungwa mkono na Marais wa Afrika kutaka mabadiliko kwa mifumo ya kutoa mikopo

Rais Ruto aliungwaa mkono na marais wa afrika alipokuwa akihutubia kongamano la Pamoja la 38 la marais wa Afrika mjini Addis Ababa Ethiopia.

Rais Ruto katika hotuba yake alielezea kutoridhishwa kwake na mifumo iliyopo  ya taasisi za kutathimini utoaji wa mikopo kwa Africa(AFCRA) alizungumza akirai kuwe na mabadiliko katika mfumo huo ambao alisisitiza kuwa iwapo kutakuwa na mabadiliko bila shaka barala la Afrika litanufika ipasavyo na litajijenga sana.

Ruto alisema kuwa kuwa mfumo wa sasa umekuwa ukinyanyasa baadhi ya mataifa ya afrika na kueneza ubaguzi kwa mataifa mengine jambo ambalo alilitaja kama unyanyasaji kwa bara la Afrika ambao hautahiki kuwepo.

Rais Ruto ambaye ni mteetezi wa mabadiliko ya Umoja wa Afrika alilalama kuwa licha ya Afrika kuwa na raslimali kubwa na nyingi limezidi kuwa bara maskini licha ya utajiri mkuu linaomiliki na  unaolikodolea macho ,alitaja kuwa Afrika ina mashamba mengi tena yenye rotuba  na raslimali yenye fulusi nyingi.

Ruto alieleza kuwa taasisi za kutoa mikopo zimetoa tu mikopo kwa mataifa mawil Afrikai tu licha ya mataifa mengi kuwa na uwezo wa kupokea na kuchangia pakubwa.

Rais Ruto alisema kuwa kama bara la Afrika wanastahili  na wanahitaji kuwe na mabadiliko iwapo shughuli hiyo ya mabadiliko katika taasisi za kutoa mikopo na sheria zitabadilika na kuwa na usawa wa haki bila shaka kama Afrika watakuwa katika mkondo mwema.

 Utafiti unaashria kuwa bara la Afrika lina uwezo wa kujisimamia kiuchumi na kimaendeleo.

‘’Utafiti unaashiria kuwa kama bara la Afrika tukijitegemea bila kuwa na mikopo Afrika inaweza zalisha dola bilioni 15.5 kiwango cha hela ambazo zinaweza kufadhili miradi maalum ya serikali zote kwa asilimia 12,huku asilimia 80 ikiangazia miundomsingi’’ Rais Ruto alieleza.

Viongozi wengine waliozungumza katika kongamano hilo la Pamoja ni Abdelmadjid Tebbounce wa Algeria,Taye Selassie wa Ethiopia,Hakainde Hichilema wa Zambia na naibu mwenyekiti wa  AUC Monique Nsanzabaganwa.

Lengo kuu la kuanzisha mfumo imara kama Afrika ni kuzindua taasisi ambayo ni ya kutathimini na kutoa mikopo kwa usawa bila ubaguzi,kuwa na uwazi wa maendeleo katika bara la Afrika na hali halisi za mataifa ya afrika, Taasisi ambayo itaangazia na kuzungumzia matatizo na matakwa ya Bara la Afrika.

Mfumo ambao ni imara kwa mataifa yote bali sio wa kutoa adhabu kwa mataifa bila kuangazia uhalisia wa mambo na vilevile taasisi ambayo inaangazia deta halisi na  kutathimini uwezo wa mataifa mengi.

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved