
Mahmoud Youssouf kutoka Djibouti amechaguliwa kuwa Mwenyekiti mpya wa Tume ya Umoja wa Afrika (AUC).
Hii ni baada ya waziri huyu wa zamani wa masuala ya kigeni kupata kura 33
Uchaguzi huo ulifanyika wakati wa Mkutano wa Umoja wa Afrika, ambapo Youssouf alimshinda wapinzani wake, Raila Odinga kutoka Kenya na Randriamandrato wa Mauritania, katika kinyang'anyiro cha ushindani mkali.
Ushindi wake unaashiria uungwaji mkono mkubwa kutoka kwa mataifa wanachama wa AU wakati anajiandaa kuongoza taasisi hiyo.
Youssouf anachukua nafasi ya Moussa Faki Mahamat, ambaye ameiongoza AUC tangu 2017, akihudumu kwa vipindi viwili mfululizo.
Uongozi wake utakuwa wa kufuatiliwa kwa karibu, kwani anakabiliwa na changamoto kuu za bara, zikiwemo ujumuishaji wa kiuchumi, vitisho vya usalama, na mageuzi ya utawala.
Akiwa mwanadiplomasia mwenye uzoefu, Youssouf, mwenye umri wa miaka 59, amehudumu kama Waziri wa Mambo ya Nje wa Djibouti tangu 2005, akicheza jukumu muhimu katika diplomasia ya kikanda na mahusiano ya kimataifa.
Anazungumza Kifaransa, Kiingereza, na Kiarabu, na ana uelewa mkubwa wa taasisi za Umoja wa Afrika, jambo linalompa nafasi nzuri ya kuongoza taasisi hiyo.
Aliyekuwa Waziri Mkuu Raila Odinga aliondolewa katika kinyang'anyiro hicho katika raundi ya saba ya upigaji kura iliyofanyika Jumamosi mjini Addis Ababa, Ethiopia.
Youssouf aliibuka mshindi wa raundi hiyo kwa kura 26, dhidi ya kura 21 za Raila baada ya raundi saba za upigaji kura katika raundi ya kwanza ya upigaji kura.
Youssouf alishinda raundi ya mwisho kwa kura 33.
Randriamandrato aliondolewa mapema, baada ya kupata kura tano katika raundi ya tatu.
Uchaguzi huo ulishuhudia nchi 49 wanachama wa AU zikishiriki huku nchi nyingine sita zikisimamishwa.
Mwenyekiti anachaguliwa na nchi wanachama, ukiondoa nchi zilizo chini ya utawala wa kijeshi.
Ilikuwa mgombea lazima apate thuluthi mbili ya kura zilizopigwa, sawa na kura 33.