logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Aliyekuwa mwenyekiti wa IEBC Wafula Chebukati ni mgonjwa mahututi

Chebukati amelazwa katika hospitali moja jijini Nairobi ambapo amekuwa akitibiwa kwa takriban wiki moja.

image
na STAR REPORTER

Yanayojiri17 February 2025 - 15:26

Muhtasari


  • Chanzo kutoka hospitalini kimesema kwamba bosi wa zamani wa IEBC amelazwa katika chumba cha wagonjwa mahututi katika hospitali hiyo.
  • Ugonjwa ambao Chebukati anaugua unasalia kuwa faragha.

IEBC Chair Wafula Chebukati.

Aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) Wafula Chebukati ni mgonjwa mahututi.

Bosi huyo wa zamani wa IEBC amelazwa katika hospitali moja jijini Nairobi ambapo amekuwa akitibiwa kwa takriban wiki moja.

Chanzo kutoka hospitalini ziliambia Radio Jambo kwamba bosi wa zamani wa IEBC amelazwa katika chumba cha wagonjwa mahututi katika hospitali hiyo.

"Tunafuatilia hali yake katika ICU," chanzo kilisema.

Ugonjwa ambao Chebukati anaugua unasalia kuwa faragha.

Chazo cha karibu cha familia kiliambia Radio Jambo kwamba bosi huyo wa zamani wa IEBC amekuwa akitibiwa nyumbani na alipelekwa katika Hospitali ya Nairobi baada ya hali kuwa mbaya.

Chebukati alihudumu kama mwenyekiti wa IEBC kwa muhula mzima wa miaka sita na alistaafu Januari 2023.

Aliongoza Uchaguzi Mkuu wa 2017 na 2022

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved