logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Onyonka, PLO waelezea sababu za Kenya kupoteza katika uchaguzi wa AUC

Sera potovu za kidiplomasia kuhusu siasa zetu za kikanda na masilahi ya mataifa mbalimbali duniani.

image
na Evans Omoto

Yanayojiri17 February 2025 - 12:19

Muhtasari


  • Kutokana na rais wa Kongo bwana  Felex Tsisekedi kususia mkutano wa ukanda wa Afrika Mashariki na kuhudhuria ule wa SADK 
  • Matamshi ya rais William Ruto miezi kadhaa iliyopita  kuhusu vita vya israeli na Palestine alinukuliwa waziwazi rais Ruto akipongeza taifa la Israeli na kuahisi Palestine usemi ambao haukuchukuliwa vyema na viongozi wa dini ya kiislamu.

Viongozi wa bara la Afrika katika ukumbi wa Nelson Mandela Ethiopia.

Baada ya kipindi cha uchaguzi wa kumtafuta mwenyekiti wa AUC kutamatika, baadhi ya wachanganuzi wa masuala ya diplomasia na kisiasa wametoa sababu za Kenya kupoteza katika uchaguzi huo.

Wachanganuzi mbalimbali wamejitokeza na kuweka bayana baadhi ya masuala ambayo huenda kama taifa hayakutiliwa maanani na kusababisha mwaniaji wa Kenya kufeli.

Seneta Richard Onyonka ambaye pia ni mtaalamu katika masuala ya kidiplomasia alipohojiwa na kituo kimoja cha Habari nchini ili aeleze kwa maoni yake chanzo kilichosababisha Kenya kupoteza katika uchaguzi wa AUC.

Bwana Onyonka alifafanua kuwa sababu ya kwanza ambayo ilichangia Kenya kupoteza katika kinyang’anyiro hicho ni kuwa na sera potovu za kidiplomasia kuhusu siasa zetu za kikanda na masilahi ya mataifa mbalimbali duniani.

Vilevile alifafanua wazi kwa kusema kuwa Vita katika taifa la Jamhuri ya Kongo pia vilichangia pakubwa ambapo rais William Ruto ndiye mwenyekiti wa ukanda wa Afrika Mashariki (EAC),alipoitisha mkutano wa Pamoja kushughulikia suala hilo ilishangaza  rais wa Kongo hakuhudhuria mkutano huo.

Kutokana na rais wa Kongo bwana  Felex Tsisekedi kususia mkutano wa ukanda wa Afrika Mashariki na kuhudhuria ule wa SADK ilikuwa ni ishara kuwa mambo hayakuwa yanaendelea vyema kutokana  na suala la kuleta amani katika taifa lake la Kongo.

Inasemekana kuwa pia katika matamshi ya rais William Ruto miezi kadhaa iliyopita  kuhusu vita vya Israeli na Palestine alinukuliwa waziwazi rais Ruto akipongeza taifa la Israeli na kuahisi Palestine usemi ambao haukuchukuliwa vyema na viongozi ambao wanaegemea dini ya kiislamu.

Jambo ambalo lilichochea mataifa yanayoegemea dini ya kiislamu kuchukua mkondo tofauti na kumpigia kura mwaniaji wa Djibout Mohamoud Ali Youssouf ambaye alikuwa mwisilamu,kutokana na kigezo hiki viongozi wengi wa mataifa mbalimbali waliamua kuchukua misimamo yao tofauti.

Wakili  PLO Lumumba  katika maoni yake alieleza kuwa  kuanguka kwa Raila katika kiti cha uenyekiti wa AUC si wa binafsi bali ni wa Taifa kwa jumla, kwani hiyo iliashiria tabia na sura ya taifa katika nchi za nje.

Vilevile alieleza kuwa ni kutokana na kufeli kwa kitengo cha masuala ya diplomasia kutofanya urafiki wa karibu uhusiano mwema na mataifa mengine ya nje akisema kuwa huo sasa ndio mwamko mpya wa kujenga uhusiano mwema na mataifa ya nje na kuteua watu bora zaidi.

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved