logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Kenya yalaumiwa na Sudani kwa kuwakaribisha waasi wa RSF

Serikali ya Sudani ilipuzilia mbali madai ya kuwa shughuli za RSF jijini Nairiobi hazikuwa na mashiko yoyote

image
na Evans Omoto

Yanayojiri20 February 2025 - 11:40

Muhtasari


  • Katika taarifa rasmi iliyotolewa na wizara ya mambo ya nje ya Sudani ilisema kuwa hio ni uvunjaji wa wajibu wa  Taifa la Kenya chini ya sheria za kimataifa.
  • Sudani ilidai kuwa Kenya ilikiuka ahadi  yake ya kuzuia shughuli za uadui dhidi ya Sudani kutoka katika ardhi yake.

Serikali ya Sudani iliikosoa vikali serikali ya Kenya kutokana na hatua yake ya kulikaribisha kuundi la waasi wa RSF kutia Saini ya makubaliano  na washirika wao jijini Nairobi.

Katika taarifa rasmi iliyotolewa na wizara ya mambo ya nje ya Sudani ilisema kuwa hio ni uvunjaji wa wajibu wa  Taifa la Kenya chini ya sheria za kimataifa,mkataba wa umoja wa mataifa ,misingi ya umoja wa Afrika na mkataba wa kuzuia uhalifu wa kimbari.

Sudani ilidai kuwa Kenya ilikiuka ahadi  yake ya kuzuia shughuli za uadui dhidi ya Sudani kutoka katika ardhi yake.

‘’Hatua hiyo ya serikali inapinga kanuni za ujirani mwema vilevile inakwenda Kinyume na ahadi zilizotolewa na Kenya katika ngazi ya juu ya kutoruhusu shughuli zozote kufanyika katika ngome yake taarifa hiyo ilieleza’’.

Serikali ya Sudani ilipuzilia mbali madai ya kuwa shughuli za RSF jijini Nairiobi hazikuwa na mashiko yoyote na kutaka jamii ya kimataifa kulaani kitendo hicho.

Wanamgambo wa RSF wamekuwa na mzozo na  serikali tawala ya Sudani na mara kwa  wamekuwa wakitishia kuuunda serikali mbadala ndani ya Sudan wakisema kuwa shughuli hiyo ingefanyikia jijini Nairobi.

Makubaliano ambayo RSF  na makundi husika yalikusudia  yawe na maafikiano ya utendakazi wa kudumu ikizingatiwa kuwa makundi ya washirika wake ambayo yana silaha  yalilenga kuunda serikali mbadala ya Amani na Umoja katika maeneo ambayo RSF inadhibiti.

Walitoa madai kuwa makubaliano na washirika wao wa karibu yalilenga utoaji wa huduma za afya,ulinzi,na kuwa na uhalali wa kuendesha shughuli zao bila matata.

Hata hivyo washikadau ambao wanahusika na mchakato huo wa utekelezaji wa mkataba huo hawakueleza makubalianao hayo yalikusudia nini ila kamati husika iliwahi sema kuwa lengo lao lilikuwa ni kurejesha serikali halali ambayo ilipinduliwa na wanamgambo wa kiislamu.

Kulingana na wao walisema hiyo ilikuwa njia moja wapo ya kujumuisha kila mmoja katika serikali ambayo itakuwa ya umoja na amani kwa uwendelevu hivyo wengi wanaliangazia suala hilo kwa ukaribu kutaka kujua ni nini kitachofuata.

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved