logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Msuada wa upokezanaji wa mamlaka ya urais wapelekwa bungeni

Msuada huo uliwasilishwa bungeni baada ya kupitishwa na baraza la mawaziri mnamo Desemba 17,2024

image
na Evans Omoto

Yanayojiri21 February 2025 - 15:10

Muhtasari


  • Msuada huo ulilenga kuweka sheria ya wazi na mchakato imara ambao utasaidia katika shughuli ya kupokezana mamlaka.
  • Msuada huo ulifafanua ukisema kuwa rais aliyoko Madarakani ataendelea au kupokeza ushindi wa mamlaka kwa rais mteule chini ya kifungu  nambari  141 ama 146 cha Katiba ya Kenya.

Kulingana na ujumbe kutoka kwa afisi ya Mkuu wa  Waziri Musalia Mudavadi msuada wa upokezaji wa mamlaka unaotarajiwa kuwasilishwa bungeni unalenga kulinda demokrasia  ya siku za usoni.

Msuada huo uliidhinishwa na baraza la  mawaziri mnamo Desemba 17,2024  na  utalainisha mchakato wa upokezanaji wa mamlaka kutoka kwa utawala mmoja hadi  mwingine bila matata.

Msuada huo unalenga kuweka sheria ya wazi na mchakato imara ambao utasaidia katika shughuli ya kupokezana mamlaka.

Lengo kuu la msuada huo ni kuhakikisha kuwa kunakuwa na uwazi na usawa wa kuchukua na kupokezana mamlaka ya urais Pamoja na sherehe ambazo zinaambatana na kuchukua hatamu  za uongozi kulingana na kifungu cha Katiba nambari 141 cha upokezenaji wa mamlaka au uongozi kabla na baada ya uchaguzi.

Msuada huo uliasisiwa na idara ya masilahi ya bunge katika ofisi ya mkuu wa mawaziri.

Msuada huo ulifafanua ukisema kuwa rais aliyoko Madarakani atapokeza mamlaka kwa rais mteule chini ya kifungu  nambari  141 ama 146 cha Katiba ya Kenya.

Naibu wa rais mteule atachukua mamlaka ya afisi chini ya kifungu cha Katiba nambari 148, mwanasheria mkuu wa serikali atachukua hatamu za uongozi kwa kulingana na kifungu cha  Katiba nambari 156 ,huku mawaziri wakila viapo vya ofisi chini ya kifungu nambari 152, huku makatibu wa kudumu katika kifungu nambari 155 huku katibu wa baraza la mawaziri akipokea kiapo chini ya kifungu 154

Mchakato wa kubadilishana hatamu za uongozi utaanza  siku tisini kabla ya kura ya rais ipigwe na  imalizike siku tisini baada ya rais mteule kuchukua hatamu za uongozi ama baada ya kamati andalizi kupeleka ripoti yake katika bunge la taifa yoyote ile itakayo tangulia.

Kamati andalizi ya mchakato huo ambayo husimamia serikali ya mpito hujumuisha watu wafuatao mkuu wa utumishi wa Umma ambaye ndiye mwenyekiti wa kamati, wanasheria mkuu wa serikali, katibu wa baraza la mawaziri, makatibu katika idara za usajili wa watu, usalama wa ndani, ulinzi, masuala ya kigeni,fedha,Habari na mawasiliano na utamaduni.

Wengine watakuwa mkuu wa majeshi,mkurugenzi mkuu wa kitengo cha ujasusi, insipekta mkuu wa polisi, karani wa bunge la kitaifa na seneti, msajili mkuu wa mahakama na wajumbe wengine tisa watakaochaguliwa na rais mteule.

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved