Mchungaji Lai ahubiri kuhusu maadili
Willifred Lai mchungaji wa kanisa la Jesus Celebration Centre liliko Bamburi Mombasa alihubiri kuhusu ufisadi,wizi naa kiburi miongoni mwa Viongozi.
Katika Mahubiri yaliohudhuriwa na viongozi wa ngazi za juu
serikalini akiwemo Rais Ruto, mchungaji Lai aliweza kuwahubiria waumini kwa
kuwaeleza maovu ambayo hutendwa na binadamu duniani.
Mchungaji aliweza kuhubiri kwa mafumbo huku akiashiria kuwalenga
watawala ambao hutumia nafasi na hadhi zao kuwadhulumu wanyonge kwa kutangaza
sera za uongo na kutowajibika ipasavyo.
Mchungaji Lai kulingana na mujibu wa mahubiri yake aliweza
kusema kuwa viongozi wale ambao wanaeleza sera za uongo na kula mali ya umma hawatafanikisha
malengo yao bali watafariki kabla ya kutimiza kile ambacho walikidai kama
kuendeleza ajenda za uongo na ufisadi.
Mchungaji Lai alisema Viongozi ambao wanadhani kuwa kukuwa tajiri
ni lazima uwe fisadi na uwaibie raia au wananchi alisema kuwa kwa kufanya hivyo
walikuwa tayari wamelaaniwa na kumuibia Mungu kwani ufalme wa Mungu si wa
wanyang’anyi.
Wakati ambapo mchungaji alikuwa anahubiria waumini waliokuwa
kanisani walionekana kuchangamkia kauli na mahubiri ya mchungaji wakisema kuwa yalikuwa
ni mahubiri na injili kali na takatifu amabayo ilikusudia kuwanyoosha wale
ambao walikuwa na mienendo potovu wabadilike.
Injili iliweza kujikita katika masuala ya ufisadi, kiburi, majigambo
na maringo mchungaji akishauri wakristo kubadilisha mienendo yao hasi ambayo
haimufurahishi Mungu, mchungaji alionekana kuwalenga wakiristo mbalimbali ambao
wamekuwa wacha Mungu ila mara nyingi wamekuwa na tabia kama za Lumbwi.
Injili ya aina hii ilikuwa ikiendelezwa na watumishi wa
Mungu kila mahali wanapokutana ili kuwawosia
viongozi kujali na kuhudumia wananchi kwa kutimiza ahadi walizo ahidi
wananchi.
Itakumbukwa kuwa askofu bwana Antony Muheria kwa wakati
mmoja alinukuliwa akitoa matamshi ya kuishauri serikali iweze kutekeleza wajibu
wake kwa kumhudumia mwananchi kwa uzalendo wa hali ya juu.
Wosia wa bwana Muheria ulipokelewa kimseto na baadhi ya viogozi serikalini
waliomkashifu kwa kuasi mambo ya dini na kuingilia siasa za taifa wakimtaka
ajiuzulu na ajitose siasani bila kuogopa