logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Maeneo ya Kenya Ambako Stima Zitapotea Leo, Jumatano - KPLC

KPLC imeonya kuhusu kukatizwa kwa umeme katika maeneo kadhaa nchini siku ya Jumatano, Februari 26, 2025.

image
na Samuel Mainajournalist

Yanayojiri26 February 2025 - 07:44

Muhtasari


  • KPLC imesema baadhi ya maeneo ya kaunti tisa za Kenya yatakosa umeme kati ya saa mbili unusu asubuhi na saa kumi na mbili jioni.
  • Kaunti ambazo zitaathirika na kukatizwa kwa umeme ni pamoja na Nairobi, Kakamega, Kisii, Embu, Meru,  Kiambu, Kitui, Kilifi, na Kwale.

KPLC

KAMPUNI ya kusambaza umeme nchini Kenya (KPLC) imeonya kuhusu kukatizwa kwa umeme katika maeneo kadhaa nchini siku ya Jumatano, Februari 26, 2025.

Katika taarifa ya siku ya Jumanne jioni, kampuni hiyo ilitangaza kwamba baadhi ya maeneo ya kaunti tisa za Kenya yatakosa umeme kati ya saa mbili unusu asubuhi na saa kumi na mbili jioni.

Kaunti ambazo zitaathirika na kukatizwa kwa umeme ni pamoja na Nairobi, Kakamega, Kisii, Embu, Meru,  Kiambu, Kitui, Kilifi, na Kwale.

Katika kaunti ya Nairobi, sehemu za maeneo ya Kangemi na UMOJA 2 zitakosa umeme kati ya saa mbili unusu na saa kumi na mbili jioni.

Soko la Lukume katika kaunti ya Kakamega litaathirika na kukatizwa kwa umeme kati ya saa tatu asubuhi na saa kumi na moja jioni.

Maeneo ya Rianyoka na Nyamasibi katika kaunti ya Kisii yataathirika kati ya saa mbili unusu na saa kumi alasiri.

Eneo la Ishiara Polytechnic katika kaunti ya Embu litaathirika kati ya saa mbili unusu na saa kumi na moja jioni.

Katika kaunti ya Meru, sehemu za maeneo ya Ntugi, Kisima, na Marania zitakosa umeme kati  ya saa mbili unusu na saa kumi na moja jioni.

Sehemu za maeneo ya Ndenderu Road, St. Linda, Gatong'ora, na Ruaka katika kaunti ya Kiambu pia zitakosa umeme kati ya saa tatu asubuhi na saa kumi na moja jioni.

Soko ya Thitani na eneo la Kanya katika kaunti ya Kitui pia zitaathirika na kukatizwa kwa umeme kati ya saa tatu asubuhi na saa kumi na moja jioni.

Maeneo ya Mwango, Mtondia, na Tezo katika kaunti ya Kilifi pia yataathirika kati yya saa tatu asubuhi na saa kumi na moja jioni.

Hospitali ya Msambweni katika kaunti ya Kwale  pia itaathirika kati ya saa tatu asubuhi na saa tisa alasiri.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved