logo

NOW ON AIR

Listen in Live

KPLC yatangaza maeneo ambayo yatakumbwa na kukatizwa kwa umeme leo, Alhamisi

Maeneo ya kaunti tisa za Kenya yatakosa umeme kati ya saa mbili asubuhi na saa kumi na moja jioni.

image
na Samuel Mainajournalist

Yanayojiri27 February 2025 - 07:03

Muhtasari


  •  KPLC imeonya kuhusu kukatizwa kwa umeme katika maeneo kadhaa nchini siku ya Alhamisi, Februari 27, 2025.
  • Kaunti zitakazoathirika ni pamoja na Nairobi, Machakos, Murang'a, Nyeri, Embu, Kirinyaga, Kakamega, Migori, na Narok.

KPLC staff at work.

KAMPUNI ya kusambaza umeme nchini Kenya (KPLC) imeonya kuhusu kukatizwa kwa umeme katika maeneo kadhaa nchini siku ya Alhamisi, Februari 27, 2025.

Katika taarifa ya siku ya Jumanne jioni, kampuni hiyo ilitangaza kwamba baadhi ya maeneo ya kaunti tisa za Kenya yatakosa umeme kati ya saa mbili asubuhi na saa kumi na moja jioni.

Kaunti ambazo zitaathirika na kukatizwa kwa umeme ni pamoja na Nairobi, Machakos, Murang'a, Nyeri, Embu, Kirinyaga, Kakamega, Migori, na Narok.

Katika kaunti ya Nairobi, sehemu za maeneo ya Kasarani, Westlands, Jogoo Road, Mombasa Road, na Kilimani zitakosa umeme kati ya saa tatu asubuhi na saa kumi na moja jjoni.

Maeneo ya soko la Mukinduri na Kiamwaki katika kaunti ya Kirinyaga  yataathirika na kukatizwa kwa umeme kati ya saa tatu asubuhi na saa kumi na moja jioni.

Maeneo ya Suswa na Duka Moja katika kaunti ya Narok yataathirika kati ya saa mbili asubuhi na saa kumi alasiri.

Soko la Makunga na lile la Lutaso katika kaunti ya Kakamega yataathirika na kukatizwa kwa umeme kati ya saa tatu asubuhi na saa kumi na moja jioni.

Katika kaunti ya Machakos, sehemu za Kangundo Road zitakosa umeme kati ya saa tatu na saa nane alasiri.

Maeneo ya Kamahuha na Makuyu katika kaunti ya Murang'a yataathirika kati ya saa tatu asubuhi na saa kumi na moja jioni.

Sehemu za maeneo ya Charity na Embaringo katika kaunti ya Nyeri zitaathirika kati ya saa mbili asubuhi na saa kumi na moja jioni.

Maeneo ya Frevane Hospital na Nthokis katika kaunti ya Embu pia yataathirika kati ya saa mbili unusu asubuhi na kumi na moja unusu alasiri.

Maeneo ya Kehancha, Ntimaru, na Taranganya katika kaunti ya Migori yataathirika kati ya saa mbili unusu asubuhi na saa kumi alasiri.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved