logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Pigo kwa Waititu huku mahakama ikikataa kumpa idhini ya kuachiliwa kwa dhamana

Mahakama Kuu imetupilia mbali ombi la aliyekuwa Gavana wa Kiambu Ferdinand Waititu la kutaka aachiliwe kwa dhamana.

image
na Japheth Nyongesa

Yanayojiri03 March 2025 - 14:12

Muhtasari


  • Jaji Njuguna pia hakukubaliana na Waititu kwamba anapaswa kuachiliwa kwa dhamana kutokana na afya yake mbaya.
  • Gavana huyo wa zamani wa kaunti ya Kiambu alipewa fursa ya kulipa faini ya Sh53.7 milioni au kutumikia kifungo cha miaka 12 jela.

Mahakama Kuu imetupilia mbali ombi la aliyekuwa Gavana wa Kiambu Ferdinand Waititu la kutaka aachiliwe kwa dhamana huku akisubiri kusikizwa na uamuzi wa rufaa yake.

Jaji Lucy Njuguna alisema muombaji huyo hakuishawishi mahakama kuwa rufaa yake ina nafasi kubwa ya kufanikiwa baada ya kusikilizwa.

"Ni maoni yangu kwamba waombaji hawajatimiza masharti ya dhamana. Maombi hayo yametupiliwa mbali," Jaji Njuguna alitoa uamuzi.
Jaji Njuguna pia hakukubaliana na Waititu kwamba anapaswa kuachiliwa kwa dhamana kutokana na afya yake mbaya.

"Baada ya kusikiliza nimepata  kwamba waombaji hawajatimiza masharti ya dhamana. Maombi hayo yametupiliwa mbali," Jaji Njuguna alitoa uamuzi.

Waititu amekuwa gerezani tangu hakimu mkuu wa mahakama ya kupambana na ufisadi Thomas Nzyoki alipomkuta na hatia ya mgongano wa maslahi ya kushughulikia makosa ya ubadhirifu wa mali na washukiwa wengine baada ya kupokea mamilioni ya pesa kutoka kaunti ya Kiambu kupitia zabuni ya barabara ya Sh588 milioni.

Gavana huyo wa zamani wa kaunti ya Kiambu alipewa fursa ya kulipa faini ya Sh53.7 milioni au kutumikia kifungo cha miaka 12 jela.

Awali, Wakili wa Waititu Danstan Omari alikuwa amewasilisha ombi katika Mahakama Kuu akitaka akubaliwe kuachiliwa  kwa dhamana ya kuridhisha akisubiri uamuzi wa rufaa aliyoiwasilisha  Waititu.

Aliiomba mahakama kuruhusu dhamana aliyoweka wakati wa kesi itumike kama dhamana inayoendelea ili kupata dhamana ya kuachiliwa kwake ambayo Ilikuwa na thamani ya Sh50 milioni wakati huo.

Gavana huyo wa zamani wa Kiambu alikuwa  amesema kuwa huenda akateseka iwapo ataendelea kusalia rumande kutokana na hali yake ya kiafya ya shinikizo la damu ambalo linahitaji matibabu ya dharura.

"Ninaamini kwamba rufaa ya hiyo ina nafasi ya kufanikiwa na kwamba nitabaguliwa ikiwa hukumu itatekelezwa," alisema.

Waititu alisema hakimu wa kesi hiyo Thomas Nzyoki alishindwa kuzingatia ushahidi wake na hakupima dhidi ya ule wa upande wa mashtaka katika kutoa hitimisho la haki.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved