logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Baadhi ya Wazee wa jamii ya Abagusii wamwidhinisha Matiang'i kuwania urais

Gusii wamuidhinisha waziri wa zamani Fred Matiang'i kuwania urais hapa nchi Kenya.

image
na Japheth Nyongesa

Yanayojiri20 March 2025 - 15:35

Muhtasari


  • Wazee hao pia walimutaja Matiang'i kama aliebadilisha mengi kwenye wizara ya teknoloja kwa wakati alipokuwa huko.
  • Vile vile wamemtaja Matiang'i kama waziri wa kujivunia wakati akiwa kwenye wizara ya usalama wa ndani.

Alikuwa waziri wa zamani wa maswala ya ndani
Kundi la wazee kutoka katika Kaunti ya kisii limekutana hii leo  Alihamisi 20 Machi na kumuidhinisha waziri wa zamani Fred Matiang'i kuwania urais hapa nchi Kenya.

Matiang'i amabaye alihudumu kama waziri wa elimu na waziri wa usalama wa ndani katika serikali iliyopita chini ya uongozi wa rais mustaafu Uhuru Kenyataa tayari ameonesha nia yake ya kuwania uongozi wa taifa.

Wazee hao wakizungumza wameeleza kwamba wao kama wazee wa Gusii pamoja na wenyeji wa eneo hilo kwa pamoja wanamwidhinisha Matiang'i anapotafuta nafasi ya kuwa rais.

"Sisi wazee wa Gusii pamoja na wenyeji tungependa kutangaza hadharani umoja wetu wa kumuunga mkono Dkt Fred Okeng'o Matiang'i anapowania ofisi kubwa kwa taifa. Kama kijana wa familia ya Gusii na ameteuliwa na watumishi wa Kenya ana historia ya kazi aliyofanya wakati wa rais Uhuru Kenyatta kwa wizari mbili ambazo alihudumu kwazo," wazee hao walisoma kauli yao.

Wazee hao pia walimutaja Matiang'i kama aliebadilisha mengi kwenye wizara ya teknoloja kwa wakati alipokuwa huko. Pia wakimpongeza kwa dhati kwa kazi ya kusifika alipohudumu kama waziri wa elimu. Wamemtaja kama aliyerejesha imani miongoni mwa mitihani ya kitaifa. pia wamemhongera kwa kuongoza kuleta tiba ya bure miongoni mwa wanafunzi na matumaini makubwa kwa vyuo vikuu.

"Kile ambacho kinajulikana sana ni wakati akiwa waziri wa elimu, alisafisha sana hasa kwenye mitihani ya kitaifa kwa kuleta  imani kwenye mitihani hiyo kwa mamilioni ya wanafunzi. Hili lilifanyika kupitia kuweka sheria kali kwa usimamizi na wanafunizi iili kuzuia wizi wa mitihani," walieleza.

Vile vile wamemtaja Matiang'i kama waziri wa kujivunia wakati akiwa kwenye wizara ya usalama wa ndani.

"Kama waziri wa usalama wa ndani Dkt Matiang'i alihakikisha usalama wa taifa uko imara kwa muendelezo muzuri wa kazi ya serikali. Aliweka uwazi Kwenye wizara ambayo ni ya muhimu sana kwenye wizara za serikali," walisisitiza wazee hao.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved