logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Shirika la ndege la Kenya KQ lapata faida ya shilingi bilioni 5.4

Shrika la ndege la Kenya KQ lilitangaza kupata faida ya shilingi bilioni 5.4 kutokana na huduma zake za usafiri

image
na Evans Omoto

Yanayojiri26 March 2025 - 09:39

Muhtasari


  • Kulingana na chapisho lake  rasmi kwenye mtandao wake wa X kampuni hiyo iliweza kutangaza kupata faida ya shilingi bilioni 5.4 baada ya kuenda hasara kwa takribani miaka 11 iliyopita.
  • Kampuni hiyo ambayo ina jumla ya ndege 35 ambazo hutua katika anga tofautitofauti za mataifa mbalimbali iliweza kurekodi faida hiyo kutokaana na usimamizi bora na utendakazi wa kufana.


Shrika la ndege la Kenya KQ lilitangaza kupata faida ya shilingi bilioni 5.4 kutokana na huduma zake za usafiri.

Kulingana na chapisho lake  rasmi kwenye mtandao wake wa X kampuni hiyo iliweza kutangaza kupata faida ya shilingi bilioni 5.4 baada ya kuenda hasara kwa takribani miaka 11 iliyopita.

Kampuni hiyo ambayo ina jumla ya ndege 35 ambazo hutua katika anga tofautitofauti za mataifa mbalimbali iliweza kurekodi faida hiyo kutokaana na usimamizi bora na utendakazi wa kufana.

Katika utendakazi wa mwaka  wa 2024 kampuni hiyo iliweza kurekodi jumla ya shilinhi bilioni 5.4 ambacho ni kiasi sawa  na dola za marekani 39.9 milioni, huku ikisafirisha abiria wengi waliosafiri kwa urefu wa miles 5.23 ambayo ni asilimia 4 huku ikibeba jumla ya tani zenye uzani wa elifu sabini na moja ambacho pia ni kiwango sawa na asilimia 25.

Kampuni hiyo vilevile iliweza kurekodi jumla ya matozo ya shiingi bilioni 188 ambacho ni kiwango sawa na dola bilioni 1.38 ambapo pia ni asilimia 6, kiwango cha huduma kwa jumla kikiwa shilingi bilioni 16.6 cha faida  lilikuwa ni ongezeko la asilimia 58 na vilevile ilipata huduma za watumishi wa ndege katika shirika hilo ikipaanda  hadi asilimia 75.2.

Kampuni hio kwa mara ya kuanza imerikodi faida hiyo baada ya kupata hasara kwa zaidi ya  miaka 11 iliyopita itakumbukwa vyema kuwa wakati  ambapo rais William  Ruto alipochukua hatamu za uongozi aliweza kusema kuwa itakuwa ni wajibu wake kuhakikisha kuwa shirika hilo  linatengeneza na kurekodi faida na kujisimammaia lenyewe.

Rais aliweza kusema hayo akilenga  kuwa kutakuwa na uongozi maalum ambao utahakikisha kuwa kila kitu kinasimama wima na kuhakikisha kuwa pesa zinatumika vyema kulingana na idadi inayoohitajika.

Mnamo mwaka wa 2023 Kampuni hiyo iliwezakutangaza kupata hasara ya shilingi bilioni 22 lakini kulingana na juhudi za usimamizi kubadilishwa na vilevile kudhibiti matumizi ya pesa katika kampuni hiyo inakadiriwa kuwa kwa muda wa mwaka mmjoa imerekodi shilingi bilioni 28 ambapo ni faida ya shilingi bilion  5.4.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved