Rais William Ruto aliwasiliana na rais wa Sudan Kusini Salvakir kuhusu tukio lililochangia Aliyekuwa Makamu wa Rais Riak Machar kukamatwa.
Baada ya mazungumzo mapana na Rais wa Uganda Yoweri Museveni na waziri mkuu Abiy wa Ethiopia Rais aliweza kuafikia maamuzi ya kutuma wajumbe wa Amani katika Taifa hilo ili kuweza kubaini chanzo cha tukio hilo na mbapo atajuzwa chanzo cha mzozo huo.
'' Nimefanya mazungunmzo na rais mwenzangu wa Uganda Museveni na Waziri mkuu wa Ethiopia Abiy na tumeafikiana kuwa nitatuma kikosi cha amani ambacho kitapiga msasa hali na kuniletea ripot kamili ya usalama huko ''. Rais Ruto alisema.
Mnamo siku ya Jumanne Rais Ruto aliweza kufanya mazungunmzo ya amani na katibu mkuu wa umoja wa kimataifa Bwana Marco Rubio kuhusu hali ya usalama katika taifa la Suadan kusini, katika mazungumzo yao walijikita sana katika hali ya kuhakikisha kuwa amani ya kudumu inajiri katika mataifa hayo mawili.
Mzozo katika taifa la Sudan kusini ulianza mnamo mwaka wa 2011 kati ya rais Salvakir na Riek Machar ambapo kulikuwa na mzozo mkali sana uliosababisha mamia na na maelifu ya raia kuuawa na kupoteza makaazi zaidi ya watu 40,000 waliweza kuuawa.
Ulipofika mwaka wa 2018 mchakato wa upatanishi na kupata suluhu ya kudumu iliweza kuanzishwa ili kuafikia hali ya amani katika taifa hilo na kuhakikisha kuwa viongozi hao wawili wanaletwa pamoja ambapo mpango huo uliweza kufanikishwa na viongozi hao wakawa wanaishi kwa amani na kwa upendo.
Hali ya kutoelewana ilianza tena hivi karibuni wakati ambapo ilisemekana kuwa Riek Machar aliweza kuuteka mji wa upper hill ambapo alionekana kushirikiana na wanajeshi Wazungu jambo ambalo lilisababisha wandani wa karibu wa Machar kuweza kukamatwa kwa kudhaniwa kuwa Machar alikuwa na njama fiche na wanajehi hao.
Jambo ambalo lilisababisha kufungiwa na jeshi katika maskani yake bila kutoka alimaarufu 'house arrest' ili kuweza kufanya uchunguzi wa kina na kubaini ukweli.
Taifa la Kenya limekuwa likishiriki katika mapatanisho ya amani katika mataifa mbalimbali na kuonyesha mchango mkubwa katika mataifa ya Afrika upatanishi wa hivi punde ni kupata suluhu ya kudumu katika taifa la DRC ambalo limekuwa na mzozo wa muda mrefu na waasi wa M23 vita ambavyo pia vimesababisha kufurushwa kwa wananchi na kuharibika kwa mali .
Kwa sasa Kenya itasubiri ripoti maalum itakayoletwa na mjumbe wa amani ili kubaini na kuelezea chanzo cha vita hivyo baada ya kuwepo kwa serikali ya pamoja ya amani kwa taifa mwaka wa 2018.