logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Sudan yasisitiza marufuku ya kutonunua bidhaa kutoka Kenya ingalipo

Taifa la Sudan lilisisitiza kuwa vikwazo vilivyowekwa vya kutonunua bidhaa kutoka taifa la Kenya vingali imara.

image
na Evans Omoto

Yanayojiri02 April 2025 - 07:58

Muhtasari


  • Katika barua yake rasmi ilioandikwa na ubalozi wake hapa nchini Kenya -Nairobi  taifa hilo lilisisitiza kuwa marufuku iliyotolewa na taifa hilo ingali imara na haijabadili nia wala msimamo kwa hilo kamwe.
  • Mnamo Machi 11,2025 wizara ya  biashara ya taifa la Sudan iliweza  kutoa amri ya kusitisha bidhaa zote zinazonunuliwa kutoka taifa la Kenya  kutokana na masilahi ya binafsi ya taifa la Sudan

Taifa la Sudan lilisisitiza kuwa vikwazo vilivyowekwa vya kutonunua bidhaa kutoka taifa la Kenya vingali imara.

Katika barua yake rasmi ilioandikwa na ubalozi wake hapa nchini Kenya -Nairobi  taifa hilo lilisisitiza kuwa marufuku iliyotolewa na taifa hilo ingali imara na haijabadili nia wala msimamo kwa hilo kamwe.

Barua hiyo iliyoandikwa ,mnamo  Aprili 1,2025 iliweza kukanusha madai na fikra kuwa mazao kutoka taifa la Kenya yangali yanauzwa katika taifa la Sudan kwa kiwango kikubwa kama ilivyokuwa hapo awali.

''Ubalozi wa  Sudan katika mji wa Nairobi ungependa kuweka mambo bayana  kuhusu kanuni za biashara za  bidhaa kutoka  taifa  la Kenya.'' Sehemu ya barua hiyo ilieleza.

Mnamo Machi 11,2025 wizara ya  biashara ya taifa la Sudan iliweza  kutoa amri ya kusitisha bidhaa zote zinazonunuliwa kutoka taifa la Kenya  kutokana na masilahi ya binafsi ya taifa la Sudan. 

''Maamuzi hayo yametekelezwa sawasawa na hakuna bidhaa zozote kutoka taifa la Kenya zimenunuliwa kufikia sasa'' aya  katika barua hiyo iliendelea kueleza.

''Taifa la Sudan linasalia imara kwa kuimarisha kanuni  zote kulingana na mujibu wake wa kidiplomasia wa biashara, na kusisitiza kuwa madai yoyote yanayosema kuwa biashara ya ununuzi wa  bidhaa kutoka Kenya inaendelea ni habari za uongo na ambazo hazijadhibitishwa ipasavyo''.

Kwa wakati huo huo Sudan ilisisitiza kupitia kwa ubalozi wake  kuwa  iko huru na ina ari kuu katika ukanda wa mataifa jumuishi katika mdahalo ambao  unaazimia kuleta umoja, ushirikiano na utangamano  kulingana na masharti  ya utunzi wa kanuni zake kwa manufaa ya mataifa yote  kwa heshima pasi mwingiliano wowote maelezo kutoka kwa barua yalifafanua.

Barua hiyo ya Ubalozi wa Sudani iliandikwa siku moja tu baada ya Rais William Ruto alipokuwa katika mahojiano na waandishi wa Habari mnamo tarehe 31 Machi ,2025 alipoulizwa na waandishi wa habari kuhusu hali  na ushirikiano wa kidiplomasia na biashara kuhusu taifa la Kenya na Sudan. 

Katika Jawabu lake Rais Ruto alisema kuwa Kenya ilikuwa ikiendelea kuuza bidhaa zake katika taifa hilo la Sudan pasi vikwazo vyovyote na kiwngo kikubwa kinachouzwa ni zao la Majani chai Rais Ruto alisema.

Marufuku ya Kibiashara kati ya Taifa la Sudan na Kenya ilitolewa  na Sudan baada ya Kenya kuwa Mwenyeji na kualika kundi haramu la Rapid  Support Forces (RSF) linalopinga utawala wa sasa wa serikali ya Sudan.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved