logo

NOW ON AIR

Listen in Live

DCI wawakamata washukiwa wawili wa wizi wa gari na ubakaji Dandora

Maafisa wa kitengo cha ujasusi DCI maeneo ya Dandora waliwakamata washukiwa wawili wa wizi

image
na Evans Omoto

Yanayojiri04 April 2025 - 10:19

Muhtasari


  • Washukiwa  hao wawili walikamatwa kwa madai ya kutekaleza vitendo hivyo vya unyama mnamo Machi 11,2025.
  • Mwathiriwa alikuwa  alikuwa akiendesha gari  katika barabara kuu ya Rua kuelekea Kangundo wakati ambapo gari lake lilipoteza mwelekeo na kukwama kando ya barabara.

Maafisa wa kitengo cha  ujasusi DCI maeneo ya  Dandora kwa ushirikiano na maafisa wa kupambana na uhalifu waliwashika washukiwa wa wizi na ubakaji.

Washukiwa  hao wawili walikamatwa kwa madai ya kutekaleza vitendo hivyo vya unyama mnamo Machi 11,2025.

Mwathiriwa mwanamke alikuwa  alikuwa akiendesha gari  katika barabara kuu ya Rua kuelekea Kangundo wakati ambapo gari lake lilipoteza mwelekeo na kukwama kando ya barabara.

Alipokuwa akifanya juhudi za kuhakikisha kuwa analiondoa  gari lake kutoka mahali lilipokwama alifikiwa na wanaume wawili waliojifaanya kuwa wanataka kumsaidia kuondoa gari hilo kutoka mahali lilipokuwa limekwama ambapo pia walikuja watu wengine watano waliojifanya kuwa wasamaria wema.

Hatimaye nia yao ilibadilika na  kumlazimisha mwenye gari kuingia katika buti ya gari na wakachukua usukani wa kuendesha gari  na kuondoka.

Washukiwa hao waliweza kuendesha gari kutumia barabara ya Kangundo kupitia Mowlem na hatimaye kusimamia karibu na mto Nairobi  kwa mbao- Dandora.

Walipofika hapo wliweza kumuondoa ndani ya  gari huku wakimpiga na kumtendea unyama huo, hatimaye kutokana na kung'ang'ana  mwathiriwa aliweza kuvutia mwendesha  gari  mmmoj aliyefika pale kutaka kujua kilichokuwa kikijiri.

Walipomwuona dereva  yule akija kutaka kujua chanzo cha mvutano huo  waliweza kuingia ndani   ya gari na kuweza kutoroka.

Baada ya kumuokoa mwathiriwa aliweza kupelekwa katika kituo cha afya ili kupata matibabu  ambapo tukio hilo liliweza kuripotiwa katika kituo cha  polisi cha kwa Mbao.

Jambo la kusikitisha na kushangaza ni kuwa mwathiriwa aliweza kupoteza vitu vyake vyote  alivyokuwa amenunua  na bidhaa zake za kimsingi na hata kuibiwa pesa zake zote kutoka kwa Akaunti zake.

 Mhasiriwa kwa sasa alikuwa katika  hali ya  unyanyapaa hio ni kutokana  na dhuluma na hali ambayo alipitia wakati alipokuwa akikumbana  na hali hio na washukiwa wale.

Aliweza kuwashukuru sana maafisa wa DCI kwa kufanya bidii na jitihada  kuhakikisha kuwa wahusika wanakamatwa  kutokana na makosa waliotenda.

Washukiwa hao waliweza kuwapeleka maafisa wa DCI katika mtaa wa Maringo Buruburu ambapo gari  lililokuwa limeibwa liliweza kupatikana  huku likiwa limeharibika.

 Ushahidi mwingine ulioweza kupatikana kutoka kwa gari la mwathiriwa liliokuwa limeibiwa .

Washukiwa kwa sasa wapo kizuizini huku wakisubiri kufikishwa mahakamani huku polisi wakiendelea na uchunguzi kubaini na kuwakamata washukiwa wengine waliokuwa katika jitihada  za kuwasaidia washukiwa hao kutekeleza wizi huo.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved