logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Rais Ruto ahudhuria kongamano la biashara duniani Nairobi

Rais Ruto alizindua kongamano la biashara duniani katika jiji kuu la Nairobi alimaarufu ''world chambers Federation African

image
na Evans Omoto

Yanayojiri09 April 2025 - 11:28

Muhtasari


  • Ni  kongamano ambalo  lilikusudia kuyaleta pamoja zaidi ya mataifa 70 kutoka kote duniani kujadili masuala ya ushirikiano wa  biashara duniani.
  • Kwa kufanya hivyo ilikuwa ni njia mojawapo ya kuhakikisha kuwa wafanyabiashara wote wanajiendeleza kuweza kupata mtaji wa kiwango ambacho wanaweza kukimudu kwa kununua bidhaa  katika mataifa mbalimbli jinsi wao wenyewe wapendavyo.

Kongamano la biashara ukanda wa Afrika la Dunia

Rais Ruto mnamo Aprili 9,2025 alizindua kongamano la biashara duniani katika jiji kuu la Nairobi alimaarufu ''world chambers Federation African Summit''.

 Ni  kongamano ambalo  lilikusudia kuyaleta pamoja zaidi ya mataifa 70 kutoka kote duniani kujadili masuala ya ushirikiano wa  biashara duniani.

 Kongamano hilo ambalo malengo yake makuu ni kuhakikisha kuwa kunakuwa na uwekezaji  mwema wa kuweza kuleta ufanisi wa biashara katika kujenga mazingira mazuri katika kuhakikisha  kuwa wawekezaji wananufaika na kupata  mazingira mema ya  kuendeshea biashara.

Kwa kufanya hivyo ilikuwa ni njia mojawapo ya kuhakikisha kuwa wafanyabiashara wote wanajiendeleza kuweza kupata mtaji wa kiwango ambacho wanaweza kukimudu kwa kununua bidhaa  katika mataifa mbalimbli jinsi wao wenyewe wapendavyo.

Rais pia aliweza kudokeza akisema kuwa kuweza kudumisha urafiki na ujirani mwema katika ulingo wa biashara bila shaka hapo utakuwa unakuza misingi na mifumo imara ambayo huweza kuleta ufanisi  mkubwa katika kukuza biashara njema  ndani ya  nchi husika.

''Kwa kuweza kuweka masikio yetu katika hali ya kuwasikiliza wajasiriamali kupitia kwa taasisi kama zile za uhasibu na viwanda  vya  kitaifa  kwa kufanya hivyo tunarahihisha wepesi wa kufanya kazi katika nchi  yetu'' Rais  aliweza kusema katika kongamano hilo.

Rais alikuwa ameandamana  na waziri wa biashara na  mikopo  ya hazina ndogondogo kwa wafanya biashara nchini Wyckliff Oparanya ambapo  muonekano wao waliweza kuhakiksha kuwa kongamamao hilo linakuwa ni la kufana sana.

Kongamano hilo liliweza kuwaleta pamoja washikadau mbalimbali katika sekta ya biashara kusudio na lengo kuu likiwa ni kuimarisha uchumi  na biashara miongoni mwa wafanyabiashara katika viwango mbalimbali.

Kongamano hilo linakusudia kuwaleta pamoja viongozi  kutoka matabaka mbalimbali,wawekezaji,wafanyabiashara  na washikadau wa serikali kutoka mataifa mbalimbali  ambapo lengo na kusudio kuu ni kuhakikisha kuwa biashara inastawi na kukuwa kote  duniani.

Kenya kwa miaka mingi imekuwa mwenyeji wa  hafla mbalimbali za  kitaifa  ili kuweza kuhakikisha kuwa mipango ya uwendelevu  kuhusu masuala mbalimbali  yanatekelezwa na kuwekwa  katika viwango vya kuheshimika si biashara  bali hata  masuala ya usalama  na hata makongamano ya kuhusu tabianchi. 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved