logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Washukiwa watatu wa wizi wa vifaa vya kielekitroniki wakamatwa Narok

Maafisa wa polisi Kutoka kituo cha polisi cha Narok waliwakamata washukiwa watatu wa wizi.

image
na Evans Omoto

Yanayojiri11 April 2025 - 16:21

Muhtasari


  • Washukiwa hao walikamatwa kwa tuhuma za  kutekeleza wizi pamoja na kusababisha vurumai katika   mji mkuu wa Narok pamoja na viunga vyake.
  • Kukamatwa huko kulitokana na wananchi kulalamikia  kuhusu hali mbaya ya usalama katika kijiji  cha Total Kaunti ya Narok.

Maafisa wa polisi Kutoka  kituo cha polisi  cha  Narok waliwakamata washukiwa watatatu wa wizi siku ya Alhamisi.

Washukiwa hao watatu  wa wizi walikamatwa kwa tuhuma za  kutekeleza wizi pamoja na kusababisha vurumai katika  mji mkuu wa Narok pamoja na viunga vyake.

Kukamatwa kwao kulitokana na wananchi kulalamikia  kuhusu hali mbaya ya usalama katika kijiji  cha Total Kaunti ya Narok.

Kwa kuweza kuzingatia na kufuatilia kwa  karibu wito wa  wananchi Maafisa wa polisi  waliweza kuwakamta washukiwa watatu ambao walikisiwa kupatikana na  vifaa vya  nyumbani waliweza kupatikana na simu za rununu, vipakatalishi na mitungi ya gesi. 

Katika vurumai hiyo mwanafunzi mmoja  wa Chuo Kikuu cha Maasai mara wa mwaka wa tatu aliweza kujeruhiwa vibaya sana kabla ya wezi hao kutekeleza wizi na kuondoka.

Kutokana na juhudi za mchwa za maafisa  wa polisi ambao walijaribu  kufuatilia tukio hilo kwa upesi  hadi   wakaweza kuwakamata washukiwa  hao watatu .

Maafisa wa usalama waliweza kupata visu vitatu vya Maasai kuashiria kuwa washukiwa hao walikuwa  na  nia mbaya ya kutaka kutekeleza maangamizi, waliweza kushikwa pia na kipakatalishi aina ya Lenovo, Simu saba,na mtungi wa  gesi wa kilo sita.

Baada ya wa washukiwa  hao kukamatwa  waliweza kuwapeleka maafisa wa polisi katika maskani yao  ambapo bidhaa zingine ziliweza kupatikana vifaaa vya kielektroniki,mtungi wa gesi,mita ya Kenya Power, na vifaa vingine vilivyoweza kupatikana na wenyewe,

Mpangaji aliyeweza kujeruhiwa aliweza kupelekwa katika hospitali ya chuo kikuu cha maasai mara kwa matibabu ambapo ilisemekana kuwa kwa  sasa hali yake inaendelea vizuri.

Washukiwa hao kwa sasa wako kizuizini wakisubiri kufikishwa kortini ila vifa ambavyo walipatikana navyo vimehifadhiwa kama ushahidi wa kutosha ili kuweza kushadidia kesi za hao washukiwa watakapofikishwa  kortini.

Visa vya wizi vimekuwa vikiripotiwa kwa  sana maeneo hayo  huku wananchi wakiwa wameripoti kuhusiana na kupotea kwa bidhaa zao huku washukiwa wakiwa katika misako mikali ya kuwakamata.

 Kwa hivyo inaashiria kuwa waliokaamatwa watakuwa sasa miongoni mwa wale wezi sugu ambao wamekuwa wakiwahangaisha wananchi na vilevile kuweza kuwaafikisha katika mahakama ili kujibu mashitaka ya wizi.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved