logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Waziri mteule wa utumishi wa Umma Geoffrey Ruku apigwa msasa katika Bunge la Taifa

Waziri mteule Geoffrey Ruku wa utumishi wa Umma alikuwa katika bunge la taifa kwa ajili ya kupigwa msasa

image
na Evans Omoto

Yanayojiri14 April 2025 - 16:09

Muhtasari


  •  Ruku ambaye alikuwa mbunge wa Mbeere Kasikazini  aliteuliwa na  rais kuweza kuhudumu katika nafasi ya waziri wa utumishi wa  umma  baada ya waziri aliyekuwepo Justine Muturi kusimamishwa  kazi na rais.
Waziri mteule katika wizara ya utumishi wa umma

Waziri  mteule Geoffrey Ruku  wa utumishi wa  Umma alikuwa  katika bunge  la taifa kwa ajili ya   kupigwa   msasa.

 Ruku ambaye alikuwa mbunge wa Mbeere Kasikazini  aliteuliwa na  rais kuweza kuhudumu katika nafasi ya waziri wa utumishi wa  umma  baada ya waziri aliyekuwepo Justine Muturi kusimamishwa  kazi na rais.

Geoffrey Ruku alihitimu masomo yake  katika chuo kikuu cha Nairobi kwa kusomea taaluma ya uhasibu mnamo mwaka wa 2008 na 2009.

Hatimaye aliweza  kujiongezea elimu kwa kusomea  taaluma  ya uhusiano mwema katka nchi za  kimataifa kama mwanadiplomasia mwaka wa 2003-2005.

Hatimaye mwaka wa 1998 hadi 2002 Ruku aliweza  kusomea taaluma ya biashara na kupata shahada hiyo katika chuo kikuu cha Catholic.

Ruku ana tajiriba pana katika safari yake ya uongozi mnamo mwaka wa 2006 na 2009 kama balozi wa Kenya nchi ya Israel, mnamo mwaka wa 2010 hadi 2011 alikuwa afisa mkuu mtebdaji wa gesi ya Kaboni Afrika.

2015 na 2017 alikuwa  afisa wa siiri  katika kampuni ya maji na uwekezaji wa hela huku mwaka wa 2013 na 2015  kama  mwanakandarAsi huru. 

Mnamo mwaka wa 2017 na 2025 hadi kama mfanyabiashra na  mshauri mkuu  ambaye amekuwa kwa jukwa katika soko kuu.

Siku ya jumatatu  ya tarehe 14 Aprili,2025  alikuwa mbele ya jopo la kumhoji ambapo aliweza kuelezea kwa kina kuhusu ufahamu wake kulingana na  zao la miraa  na  mugoka ikikisudiwa  kuwa  kule  alikotoka ndiko kitovu  cha zao hilo.

Alikuwa  anajibu swali ambalo mheshimiwa  Baya alitaka aelezee bunge wakati  ambapo alikuwa  katika kamati hiyo ya kilimo akiwa mbunge ilibainika kuwa  aliweza  kuchochoea mabadiliko ambayo wabunge  walitaka ufahamu ni kwa nini alifanya hivyo na vilevile wabunge  walitaka  kujua tofauti ya  miraa na Mugoka.

Aliweza kusema kuwa miraa na Mogoka  ni mimea ambayo inapatikana  katika familia moja  ya kisanzi ila tofauti ni kidogo kulingana na asili yake  ya  mwanzo .

Aliweza kukariri kwa  kusema kuwa  zao la miraa na mugoka lilikuwa likipandwa katika sehemu mbalimbali za  taifa wala si sehemu moja tu jinsi ambavyo wengi walivyodadisi alisema kuwa miraa ilipandwa maeneo ya Meru, embu, Muranga, Machakosi na  sehemu za Makueni.

 Aliweza kusema kuwa miraa na mogaka ilikuwa na athari chanya  za  kiaya  kwa  watu kando na madai ya watu kuwa zao hilo ni baya kwa  afya ya binadamu.

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved