logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Wizara ya afya kuanzisha uchunguzi katika hospitali ya Medheal Eldoret kwa madai ya uuzaji wa figo

Wizara ya afya ilipokea barua kutoka kwa muungano wa umma ikitaka uchunguzi kuhusu uhamishaji wa vuioungo ufanywe

image
na Evans Omoto

Yanayojiri16 April 2025 - 08:32

Muhtasari


  • Barua hiyo iliweza kuelezea ongezeko kuu la uuzaji wa figo kwa  taifa  la Israel,Jamii iliweza kushuku pakubwa ongezeko la watu kujitolea kwa ajili ya kuuza  viungo vyao huku  likitilia shaka uwezekano wa  kuvunjwa  kwa sheria za afya  nchini.

Health CS Aden Duale 

Wizara ya afya ilipokea  barua  kutoka kwa afisi inatoa huduma za uhamishaji wa   viungo  vya  mwili iliyoandikwa 20 Julai 2023 kwa  madai ya  uuzaji wa viungo vya mwili.

Barua hiyo iliweza kuelezea ongezeko kuu la uuzaji wa figo kwa  taifa  la Israel,Jamii iliweza kushuku pakubwa ongezeko la watu kujitolea kwa ajili ya kuuza  viungo vyao huku  likitilia shaka uwezekano wa  kuvunjwa  kwa sheria za afya  nchini.

Kulikuwa na taarifa  za  kuaminika kuwa uuzaji wa viungo vya  mwili  hasa figo vilikuwa  vimekithiri ambapo mfadhili mkuu wa zoezi  hilo alikuwa  anatoka Israel ambapo alikuwa anashirikiana na hospitali ya Mediheal Eldoret.

Kutokana  na tetesi hiizo wizara iliweza  kuanzisha uchunguzi wa haraka kwa kuunda  jopo la uchunguzi lililoshirikisha timu ya kamati  ya upelelezi na   adhabu   iliyowajumuisha wataaalamu kutoka kwa kitengo cha  madili,idara ya uhamishaji wa viungo  vya  mwili,mwakilishi kutoka kwa idara ya utoaji wa damu, waakilishi kutoka kwa muungano wa kutetea  maslahi ya madktari, wawakilishi kutoka kwa wizara  ya Afya  na wawakilishi kutoka kwa  muungano wa  madaktari wa Meno.

 Jopo hilo lilianzisha kwa haraka utafiti wa haraka ili  kubaini ukweli wa madai hayo yaliyokuwa yameenea kwa  kiwango kikubwa  kwanzia tarehe 5  hadi 8 Disemba 2023.

Majukumu ya   jopo hilo yalikuwa  ni kuhakikisha  kuwa  yanahakiki madai yaliyoibuliwa  na shirika la ubadilishaji wa viungo,  kutathimini  jinsi ya kubadilisha viungo hivyo katika hospitali hizo katika  hospitali na  kupendekeza hatua ambazo zinastahili kuchukuliwa baada ya uchunguzi kutamatika  na ripoti ya  matokeo kutolewa.

Jopo liliweza kutathimini   na kutaja  vitengo muhimu ambavyo lilipanga  kuja kuvishughulikia  kwa mfano kuendeleza utoaji wa figo na jinsi ya kutoa moja kwa  moja, kupiga tathimini ya muendelezo huo katika hospitali ya Mediheal  hasa upande  wa kubadilishaji wa viungo.Kuhakikisha kuwa inahitimisha ripoti na  hatimaye kutoa mapendekezo kwa  wizara  ya afya.

Kulingana na matokeo ya jopo ni kuwa  ilibainika kuwa Hospitali ya Mediheal  ilikuwa ni hospitali ambayo ilikuwa  katika mji wa Eldoret na ambayo  iko katika  kiwango cha level 5 na  ambayo iliidhinishwa kwanza kufanya operesheni kadhaaa  za  kuhamisha  viungo    vya  mwili na ilikuwa  ikifanya hivyo kwa zaidi ya miaka mitano   iliyopita na ambapo jumla ya visa vya  uhamishaaji wa viungo 372 vilikuwa vimetekelezwa.

ilibainika pia kuwa hospitali hiyo ilikuwa  imefanya shughuli hiyo kwa zaidi ya mataifa matano afrika mashariki  Kenya,uganda,Burundi, Ethiopia ,DRC, Somalia na na mataifa ya ulaya kama Australia, Israel, Japan, USA na  UK.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved