logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Hongera Atletico!!- Mabingwa wa Laliga 2020/2021

Atletico Madrid imeshinda kombe la Laliga na pointi 86 ikifuatwa kwa karibu na Real Madrid, 84, na Barcelona ,79.

image
na Radio Jambo

Habari22 May 2021 - 18:22

Muhtasari


•Atletico Madrid imeshinda kombe la Laliga na pointi 86 ikifuatwa kwa karibu na Real Madrid, 84, na Barcelona ,79.

Wachezaji na na kocha wa Atletico washerehekea

Klabu ya Atletico Madrid imeibuka mshindi wa kombe la Uhispania almaarufu kama Laliga.

Atletico ilishinda kombe hilo siku ya Jumamosi baada ya kucharaza Real Valladoid mabao mawili kwa moja na kujihakikishia nafasi hiyo ya kileleni. Mabao ya Atletico yalifungwa na Correa na Luiz Suarez huku Oscar Plano akifungia Valladoid.

Klabu hiyo inayoongozwa na Diego Simeone iliweza kuzoa alama 86 msimu huu huku ikifuatwa nyuma kwa karibu na mahasidi wa jadi Real Madrid na Barcelona zikijizolea alama 84 na 79 mtawalia.

Hii ni mara ya 11 klabu hiyo kushinda kombe la Laliga huku ikishinda mara ya mwisho msimu wa 2013/2014.

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved