logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Hamilton amsifu Kipchoge mbele ya mbio za Berlin

Kipchoge atakuwa akirejea Berlin Marathon kwa mara ya kwanza baada ya miaka minne.

image
na Radio Jambo

Habari24 September 2022 - 17:27

Muhtasari


  • Hamilton alisema katika ujumbe wa video uliorekodiwa awali kwamba alijua kazi kubwa ambayo Kipchoge anakabili
Eliud Kipchoge baada ya kushinda dhahabu usiku wa kuamkia Jumapili

Bingwa wa Multiple Formula One Lewis Hamilton ametuma ujumbe wa kutia moyo kwa bingwa mara mbili wa Olimpiki wa marathon na mshikilizi wa rekodi ya dunia Eliud Kipchoge kabla ya mbio za Berlin siku ya Jumapili.

Hamilton alisema katika ujumbe wa video uliorekodiwa awali kwamba alijua kazi kubwa ambayo Kipchoge anakabili.

"Nilitaka tu kukutumia ujumbe wa kukutakia kila la kheri katika juhudi zako zote zijazo. Najua una shabaha kubwa inayokuja kwenye Berlin Marathon, nitakuwa nikifuatilia kwa karibu,” Hamilton alisema.

Hamilton alimlimbikizia Kipchoge sifa, akisema alifurahia uwezo wake usio na kifani wa kuvunja dari za vioo.

"Nimehamasishwa na jinsi unavyoendelea kusukuma na kuonyesha kuwa hakuna mipaka isipokuwa ile tuliyoweka akilini mwetu. Endelea kuwa na ndoto kubwa, endelea kusukuma, bahati nzuri na ninakutakia kila la heri,” Hamilton alisema.

Kipchoge atakuwa akirejea Berlin Marathon kwa mara ya kwanza baada ya miaka minne.

“Nataka kukimbia mbio nzuri. Mbio nzuri ni mbio nzuri. Ni mbio ambazo kila mtu hukimbia huku akiwa na furaha.

Kipchoge analenga kuvunja rekodi ya dunia (2:01.39) aliyoweka mwaka wa 2018.

"Ikiwa nitakimbia na kuishia kuvunja rekodi, basi itakuwa mbio nzuri," alisema


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved