logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mkenya Peres Chepchirchir avunja rekodi ya mbio za London marathon

Chepchirchir aliandikisha muda wa saa mbili dakika 16 na sekunde 16.

image
na Radio Jambo

Habari22 April 2024 - 03:58

Muhtasari


•Chepchirchir aliandikisha muda wa saa mbili dakika 16 na sekunde 16 katika mbio hizo ambapo waliomaliza wanne bora walishinda rekodi pekee ya awali ya wanawake ya saa 2:17:01.

Bingwa wa Olimpiki Peres Jepchirchir wa Kenya amevunja rekodi ya pekee ya dunia ya wanawake katika mbio za London marathon.

Chepchirchir aliandikisha muda wa saa mbili dakika 16 na sekunde 16 katika mbio hizo ambapo waliomaliza wanne bora walishinda rekodi pekee ya awali ya wanawake ya saa 2:17:01 iliyowekwa na Mkenya Mary Keitany mnamo 2017.

Tigst Assefa wa Ethiopia alikuwa wa pili huku Joyciline Jepkosgei wa Kenya akiwa wa tatu.

Mkenya Alexander Mutiso Munyao alimshinda bingwa wa mbio za masafa marefu Kenenisa Bekele na kushinda mbio hizo upande wa wanaume kwa saa 2:04:01.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved