logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Kocha Bonface Ambani alalamikia wizara kuwahongera Rising Stars kwa shilingi milioni 1.8

Rising Star walizawadiwa hela hizo baada ya kufuzu AFCON ya wavulana waiozidi umri wa miaka 20 itakayochezwa 2025

image
na Brandon Asiema

Michezo23 October 2024 - 11:36

Muhtasari


  •  Ambani amemtaka waziri Murkomen kuwacha kufanya utani na vijana hao wa Rising Stars akistaajabia zawadi murwa wizara ya michezo inaweza wapa wachezaji hao ni shilingi milioni 1.8 pekee.
  • Rising Stars walirejea nchini siku nya Jumatatu 21, baada ya kukamilisha mechi za kufuzu AFCON ukanda wa CECAFA

Kocha wa klabu ya Mara Sugar inayoshiriki ligi kuu nchini Kenya Bonface Ambani amekashifu hatua ya waziri wa michezo Kipchumba Murkomen kuwazawidi wachezaji wa timu ya wavulana ya taifa ya Kenya wasiozidi umri wa miaka 20 kitita cha shilingi milioni 1.8.

Timu hiyo baada ya kulakiwa katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa JKIA mnamo Jumatatu, waliandaliwa staftahi siku ya Jumanne katika jumba la Talanta kuwasherehekea kutokana na kufuzu mashindano ya AFCON yatakayoandaliwa nchini Afrika Kusini mwaka wa 2025.

Kulingana na Ambani, amemtaka waziri Murkomen kuwacha kufanya utani na vijana hao wa Rising Stars akistaajabia zawadi murwa wizara ya michezo inaweza wapa wachezaji hao ni shilingi milioni 1.8 pekee.

“Ikiwa watagawana shilingi hizo pamoja na benchi la kiufundi, hiyo ni chini ya 40K… hii serikali inaweza kufanya vyema Zaidi ys hii.” Alimaka Ambani kwenye ukurasa wake wa Meta.

Mchezaji huyo wa zamani wa timu ya taifa ya Kenya Harambee Stars, alisikitikia kuwa baada ya wiki mbili ya vijana wa Rising Stars kuweka kambi nchini Tanzania kwa ajili ya bendera ya taifa, kitu cha pekee serikali ya Kenya inaweza kuwapa ni shilingi 40,000.

“Serikali inaweza fanya zaidi ya hii, ni nini mbaya na hawa maafisa wa serikali. Wiki mbili na Zaidi nje ya nchi, kitu pekee wavulana hawa wanapewa ni elfu 40.” Aliandika kocha Ambani.

Bonface Ambani amewataka maafisa katika wizara ya michezo kuwacha utani huo akisema kuwa wachezaji na benchi la kiufundi wanastahili mazuri zaidi ya walichopewa.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved