logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Kampuni ya Adidas yazindua kiatu chenye sahihi ya Lamine Yamal

Kampuni ya Adidas imetangaza kiatu chake cha kwanza kabisa cha kutia saini kwa mchezaji mchanga wa uhispania Lamine Yamal

image
na OTIENO TONNY

Michezo17 December 2024 - 12:11

Muhtasari


  • Kiatu hicho kimeundwa na Kampuni ya Adidas kwa ushirikiano na Lmine Yamal.
  • Lamine alichagua rangi ya pinki kutumika kwenye kiatu hicho akisema kuwa ni mojawapo wa rangi anazozipenda zaidi.



Kampuni ya kutengeneza mavazi ya Adidas imezindua kiatu chenye sahihi ya mchezajikinda wa Barcelona Lamine Yamal kama njia ya kusherehekea ufanisi wa mwanasoka huyo.

Uzinduzi wa kiatu hicho kinatokana na kuhitimu kwa Yamala katika shule ya upili na kufika kileleta kwa mashindanoya UEFA EURO ambapo timu yake ya taifa la Uhispania ilitinga fainali ya mashindano hayo.

Kiatu hicho kilichotengenezwa na kampuni ya Adidas  kina sifa za kuvutia macho kutokana na ustadi uliotumika kukitengeneza kikiashiria ubora wa mchezaji huyo aliyetajwa kuwa bora wa chini wa umri wa miaka 21 barani Ulaya mwaka 2024.

Katika mwenokano wa kiatu hicho, Lamine alichagua rangi ya zambarau ambao ni mojawapo wa rangi anazozipenda  ila nembo F50 kwenye ngozi ya kiatu hicho ikibadilishwa na tarakimu tatu za mwisho za nembo ya nambari za  posta wa mji wa nyumbani anakotoka Yamal ambayo ni  304 iliyoandikwa kwa rangi ya dhahabu. Mwonekano huo umetumika kuonyesha heshima kwa jamii ambayo imemtazama akiwa  mtoto mchanga mpaka  akibadilika na kuwa kipaji cha kizazi.

Akiongea kuhusu ushirikiano wake na Kampuni ya Adidas Lamine alisema kuwa tukio hilo limekuwa kama ndoto kwa maisha yake.

"Mwaka huu umekuwa kama ndoto kwangu, na kufanya kazi na adidas kwenye kiatu changu cha kwanza iliyosainiwa imekuwa nzuri sana. Waliponialika kufanya kazi na wabunifu na kuwa miongoni mwa walioiunda kiatu hicho, nilifurahi sana kuona jinsi ilivyoundwa,’’ Alisema Lamine

Adidas walisherehekea uzinduzi huo kwa kupiga picha maalum huku  Lamine Yamal akiwa amevalia mavazi ya rangi ya waridi ya kuhitimu. Lamine alikiri kuwa anapenda rangi ya pinki.

‘’Pinki ni mojawapo ya rangi ninazozipenda, na mimi ni mchezaji ambaye hupenda kuleta umaridadi uwanjani, kwa hivyo ilikuwa muhimu kwangu kwamba rangi hilo litumike,’’ Aliongezea Yamal.

Sam Handy, Meneja Mkuu wa Soka katika Kampuni wa Adidas, alisema kuwa ni vigumu kwa wachezaji wengi kuwa miongoni mwa wale wanaoshirikiana katika shughuli kama hiyo.

 "Tunapozungumzia wachezaji ambao wana saini zao za kiatu cha adidas, tunaangalia majina machache tu ambayo yamefikia kiwango hicho cha uwezo na umaarufu,’’ Alisema Handy.

Ikiwa ni jozi 304 pekee zinazopatikana kununua duniani kote, kifurushi cha adidas F50 LY304 kinaweza kununuliwa kuanzia Desemba 18.


 



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved