logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Ronaldo kugombea urais wa shirikisho la soka la Brazil

Nyota huyo atawania urais wa CBF ili akipania kuchukua nafasi ya rais wa sasa Ednaldo Rodrigues katika mwaka wa 2026.

image
na OTIENO TONNY

Michezo17 December 2024 - 16:33

Muhtasari


  • Ronaldo aahidi kuibadilisha soka la Brazil 
  • Ameongeza kuwa brazil inawachezaji wazuri wengi wanaoweza kulisaidia timu hiyo kupata ushindi.

caption

Mshambulizi wa zamani wa Brazil Ronaldo atawania kiti cha urais wa shirikisho la soka nchini humo (CBF), mchezaji huyo sasa ana umri wa miaka 48.

Ronaldo, ambaye alishinda Kombe la Dunia akiwa na Brazil mwaka 1994 na 2002, atagombea kama mgombea katika uchaguzi wa CBF ili kuchukua nafasi ya rais wa sasa Ednaldo Rodrigues katika mwaka wa  2026.

Ronaldo alisema kuwa anasumbuliwa na hali ya watu wengi wa nchi hiyo ya Brazil ambao sasa hawana upendo kwa timu hiyo ya Taifa.

‘’Miongoni mwa mamia ya mambo yanayonitia moyo kuwa mgombea urais wa CBF ni kurejesha umaarufu na heshima ambayo timu hii ya taifa imekuwa nayo siku zote na ambayo hakuna mtu mwingine aliye nayo leo.” Alisema Ronaldo.

Brazil wameshinda Copa America mara moja tangu Ronaldo alipostaafu katika michezo za kimataifa mwaka wa 2011 na kutolewa nje ya Kombe la Dunia la 2022 na Croatia katika robo fainali.

Nyota huyo wa kitambo aligadhabishwa na matokeo mabaya ya timu hiyo ya brazil licha ya kuwa na baadhi ya wachezaji bora zaidi ikiwemo Vinicius Junior, Estevao  na Endrick.

‘’Tuna wachezaji bora, tuna Vinicius Junior, Neymar, Rodrygo, Estevao na  Endrick miongoni mwa wengine wengi,  tuna vipaji vingi, tunawezaje kutocheza vizuri tukiwa na hawa wote,’’ Alisema Ronaldo.

Mshambulizi huyo wa zamani wa Barcelona, ​​Inter Milan na Real Madrid kwa sasa pia alisema anatarajia kuuza dau lake katika klabu inayoshiriki ligi kuu ya Uhispania Real Valladolid.

‘’Tunafanya mazungumzo ya uwezekano wa kuuza hivi karibuni na tunapaswa kufunga mpango huo. Haitakuwa kikwazo kwa ugombea wangu," Alisema nyota huyo.

Muhula wa Rodrigues utaendelea hadi Machi 2026 na uchaguzi wa urais lazima ufanyike katika miezi 12 kabla ya wakati huo.




RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved