logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Amad Diallo arefusha mkataba na Manchester United

Mkataba mpya ni wa miaka mitano na nusu ambapo utakamilika Juni, 2030.

image
na Brandon Asiema

Michezo10 January 2025 - 08:19

Muhtasari


  • Diallo amesema  ana matumaini ya kuandikisha historia katika klabu ya Manchester United.
  • Mkataba wa awali wa Diallo ulikuwa unakamilika mwishoni wa msimu huu na ulikuwa na kipengee cha Man United kurefusha kwa mwaka mmoja.


Winga wa Manchnester United Amad Diallo ametia sahihi mkataba mpya na miamba hao wa soka wa jiji la Manchester wa miaka mitano na nusu. Mkataba huo utamfikisha hadi mwaka wa 2030 mwezi Juni.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 22 raia wa Ivory Coast ameelezea furaha ya kuwepo kwa mkataba mpya na Man United. Mkataba wa awali ulikuwa unakaribia kikomo ambapo unakamilika mwisoni mwa msimu huu.

Diallo amekuwa kwenye ubora tangu tangu kujiunga na klabu hiyo mnamo mwaka wa 2021 akiwa amefunga mabao tisa katika mechi 50 alizoshiriki.

"Ninajivunia kusaini mkataba huu mpya. Nimekuwa na nyakati za ajabu na klabu hii tayari lakini kuna mengi zaidi yanakuja," Alisema Diallo baada ya kutia sahihi mkataba huo mpya.

Katika malengo yake baada ya kutia sahihi mkataba  huo  mpya, Diallo amesema kwamba ana matumaini ya kuandikisha historia katika klabu hiyo kwenye miaka atakayokuwa anatumikia klabu hiyo.

Vile vile, amekiri kuwa Manchester United inakabiliwa na wakati mgumu haswa msimu huu akiadhidi kujitolea kuisaidias kurejesha adhi ya timu hiyo.

"Nina matarajio makubwa kwenye mchezo na ninataka kuweka historia katika Manchester United. Umekuwa msimu mgumu kwa kila mtu, lakini ninaamini kabisa kwamba tuko kwenye njia sahihi na siku zijazo zitakuwa nzuri. Niko tayari kutoa kila kitu kusaidia timu na kuwafanya mashabiki wetu wajivunie tena." Aliongeza Diallo.

Fomu ya Amad Diallo imekuwa njema huku hivi karibuni akisaidia Man United kupata bao muhimu la kusawazisha kwenye mechi ya ligi dhidi ya Liverpool.

Diallo alisalia kambini Old Trafford wakati wa kocha aliyetimuliwa Erik Ten Hag wakati ambapo kulikuwepo na uwezekano wa kuondoka msimu uliopita.



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved