logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Barcelona Yaipiga Real Madrid Fainalini Licha Ya Kipa Kuonyeshwa Nyekundu

Barca walisalia na wachezaji 10 pale kipa Wojciech Szczesny alipotolewa kwa kadi nyekundu kwa kumchezea vibaya Mbappé

image
na MOSES SAGWEjournalist

Michezo13 January 2025 - 07:47

Muhtasari


  • Lakini kile kilichoonekana kama mwanzo wa ndoto haraka kiligeuka kuwa jinamizi kwa vijana wa Ancelotti wakati Yamal alipoisawazishia Barca dakika ya 22.
  • Mshambulizi Lewandowski aliwapatia bao la kuongoza dakika 14 baadaye kwa mkwaju wa penalti uliotolewa kwa Eduardo Camavinga kumchezea rafu Gavi.



BARCELONA walitoka nyuma kwa kuufngwa bao la mapema na kuwalaza Real Madrid 5-2 katika fainali ya Spanish Super Cup Jumapili, wakifunga mabao manne katika kipindi cha kwanza na kunusurika baada ya mlinda mlango wao kutolewa nje kwa kadi nyekundu na kunyakua rekodi ya 15 ya kombe hilo.


Lamine Yamal, Robert Lewandowski, Raphinha na Alejandro Balde wote walilenga lango kabla ya kipindi cha mapumziko, baada ya fowadi wa Ufaransa Kylian Mbappé kuweka Real mbele dakika ya tano.


Raphinha alifunga jingine kipindi cha pili huku Rodrygo akiifungia Real.


Barcelona walifanya maonyesho ya kipekee kunyanyua taji lao la kwanza ndani ya zaidi ya mwaka mmoja, wakiwa hawana fedha za kuonyesha msimu uliopita.


"Lengo kwa vilabu vikubwa siku zote ni kushinda mataji, ndiyo maana tunafanya kazi kwa bidii. Lakini sasa lazima tuonyeshe katika michezo inayofuata," Hansi Flick aliambia mkutano wa wanahabari baada ya kushinda taji lake la kwanza kama mkufunzi wa Barca.


"Real ilifanya makosa mengi, na tulijua jinsi ya kuchukua faida yao kudhibiti mechi."


Barca waliizuia Madrid kushinda taji lao la tatu la kampeni, baada ya kushinda Kombe la Super Cup la Uropa dhidi ya Atalanta na kuwashinda Pachuca ya Mexico hadi Kombe la Intercontinental mwezi uliopita.


"Katika kipindi cha kwanza hatukucheza soka, tulipiga mipira mirefu na hilo halikuwa wazo," kocha wa Madrid Carlo Ancelotti alisema.


"Niliwaambia wachezaji kwamba wanaweza kupoteza michezo, lakini si kwa jinsi tulivyocheza katika kipindi cha kwanza."


Mbappé alipata faida ya mapema kwa mabingwa wa Uhispania, akimalizia mbio za pekee kutoka karibu na mstari wa nusu kwa shuti ndani ya nguzo ya mbali.


Lakini kile kilichoonekana kama mwanzo wa ndoto haraka kiligeuka kuwa jinamizi kwa vijana wa Ancelotti wakati Yamal alipoisawazishia Barca dakika ya 22.


Mshambulizi Lewandowski aliwapatia bao la kuongoza dakika 14 baadaye kwa mkwaju wa penalti uliotolewa kwa Eduardo Camavinga kumchezea rafu Gavi.


Raphinha aliongeza bao hilo kwa mpira wa kichwa mzuri kutoka kwa krosi ndefu iliyopigwa na Jules Koundé dakika ya 39, na beki wa kushoto Balde aliongeza bao la nne kwa Barca dakika za lala salama baada ya dakika tisa kuongezwa kipindi cha kwanza.


Yamal alimtoa Raphinha kwa pasi sahihi kufuatia mpira wa kona mbaya wa Madrid, kabla ya fowadi huyo wa Brazil kumuachia mpira Balde ambaye alifunga kwa kumalizia kirahisi.


Madrid walianza kipindi cha pili huku Rodrygo akipiga lango, na hivyo kuzua matumaini ya mpambano huo mkali kuchukua zamu nyingine.


Lakini Raphinha alizima mvutano wowote wa kurejea alipofanya matokeo kuwa 5-1 dakika tatu baada ya mapumziko, baada ya kuwachambua walinzi wa Madrid.


Barca walisalia na wachezaji 10 pale kipa Wojciech Szczesny alipotolewa kwa kadi nyekundu kwa kumchezea vibaya Mbappé dakika ya 56 na Rodrygo akamshinda kipa Iñaki Peña kutokana na mpira wa adhabu uliotokana na matokeo.



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved