logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Real Vs Atletico; Liverpool Vs PSG…Mechi Za Kukata Na Shoka Raundi Ya16 UCL

Liverpool itacheza na Paris Saint-Germain katika hatua ya 16 bora ya Ligi ya Mabingwa huku Arsenal ikimenyana na PSV Eindhoven na Aston Villa kumenyana na Club Brugge.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Michezo21 February 2025 - 16:09

Muhtasari


  • Timu zote tatu za Uingereza ziko upande mmoja wa droo hiyo ikimaanisha kuwa Liverpool wanaweza kukutana na Aston Villa katika robo fainali kisha Arsenal katika nusu fainali.
  • Klabu yoyote ya Uingereza inayotarajia kutinga fainali inaweza kukutana na mabingwa Real Madrid lakini hawatacheza na Barcelona hadi fainali.

Liverpool kukutana na PSG huku Real Madrid ikikutana na Atletico de Madrid

Liverpool itacheza na Paris Saint-Germain katika hatua ya 16 bora ya Ligi ya Mabingwa huku Arsenal ikimenyana na PSV Eindhoven na Aston Villa kumenyana na Club Brugge.

Mechi za hatua ya 16 bora zitafanyika Machi 4 na 5 huku mechi za mkondo wa pili zikichezwa Machi 11 na 12.

Timu zote tatu za Uingereza ziko upande mmoja wa droo hiyo ikimaanisha kuwa Liverpool wanaweza kukutana na Aston Villa katika robo fainali kisha Arsenal katika nusu fainali.

Klabu yoyote ya Uingereza inayotarajia kutinga fainali inaweza kukutana na mabingwa Real Madrid lakini hawatacheza na Barcelona hadi fainali.

Liverpool walimaliza kileleni mwa awamu ya ligi huku PSG wakifuzu kupitia hatua ya mtoano kwa ushindi wa kushangaza wa 10-0 dhidi ya Brest.

Arsenal walifanikiwa kufuzu katika mechi ya tatu wakitoka sare ya bila kufungana dhidi ya PSV, ambao waliwatoa Juventus kwenye mechi ya mtoano kwa ushindi wa 3-1 wa mkondo wa pili na kushinda kwa jumla ya 4-3.

Aston Villa ilinyakua nafasi ya mwisho ya kufuzu moja kwa moja na sasa itamenyana na Club Brugge baada ya kuishinda Atalanta kwa ushindi wa jumla wa 5-2.

Hii hapa droo kamili ya mechi hizo;

1.       Borussia Dortmund dhidi ya Lille

 

2.       Real Madrid vs Atletico Madrid

 

3.       Bayern Munich vs Bayer Leverkusen

 

4.       PSV Eindhoven vs Arsenal

 

5.       Feyenoord dhidi ya Inter Milan

 

6.       Paris Saint-Germain vs Liverpool

 

7.       Benfica vs Barcelona

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved