logo

NOW ON AIR

Listen in Live

“Ligi Haiko Mikononi Mwetu Tena!” Arteta Asema Baada Ya Liverpool Kushinda

"Haipo mikononi mwetu. Kwangu mimi, kwa kweli, nimekerwa sana na mambo ambayo yalikuwa mikononi mwetu ambayo hatukufanya vizuri tulivyoweza na huo ndio uchezaji," Arteta alisema.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Michezo24 February 2025 - 08:30

Muhtasari


  • Bao la Jarrod Bowen lilitosha kwa wagonga nyundo hao kutwaa pointi zote tatu kwenye Uwanja wa Emirates,
  • Kazi ya Arteta imefanywa kuwa ngumu zaidi na majeraha kwa Kai Havertz na Gabriel Jesus. 

Mikel Arteta

KOCHA wa Arsenal, Mikel Arteta amesema kwa kutamauka kwamba mbio za klabu hiyo kung’ang’ania ubingwa wa ligi ya Premia, EPL msimu huu zimepata pigo kubwa baada ya wao kushidnwa dhidi ya West Ham na washindani wao Liverpool kushinda dhidi ya Manchester City.

Arteta ambaye alionekana kuwa na hasira, alisema kwamba ligi ya EPL sasa haiko mikononi mwao kama ambavyo walikuwa wanatarajia kwani sasa Liverpool imefungua pengo la alama 11 kileleni.

"Haipo mikononi mwetu. Kwangu mimi, kwa kweli, nimekerwa sana na mambo ambayo yalikuwa mikononi mwetu ambayo hatukufanya vizuri tulivyoweza na huo ndio uchezaji," Arteta alisema.

"Tumekatishwa tamaa sana, ni wazi pia kuwa na hasira. Lazima tuwe na hasira. Natumai tuko sana kwa sababu hatukufikia viwango leo na ninawajibika sana, na nina hasira sana.”

"Nadhani tunapaswa kuwapongeza West Ham kwa ushindi na mchezo ambao walicheza lakini nadhani mengi kwa upande wetu hatujawahi kuwa sawa. Ni jukumu langu kwa timu kucheza vizuri zaidi kuliko ilivyocheza leo."

Kichapo cha Jumamosi dhidi ya West Ham kimewaacha The Gunners kwa pointi 11 na vinara Liverpool waliokimbia. Ingawa wana mchezo mkononi dhidi ya Wekundu hao, itakuwa ni jambo la kawaida iwapo Arsenal itamaliza kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya England mwishoni mwa msimu huu.

Bao la Jarrod Bowen lilitosha kwa wagonga nyundo hao kutwaa pointi zote tatu kwenye Uwanja wa Emirates, huku Arsenal nao wakishuhudia Myles Lewis-Skelly akitolewa kwa kadi nyekundu. Kazi ya Arteta imefanywa kuwa ngumu zaidi na majeraha kwa Kai Havertz na Gabriel Jesus.

Na jukumu la Mhispania huyo sasa limewekwa wazi na nyota wa Liverpool, Michael Owen. Mshambulizi huyo wa zamani amesisitiza kuwa The Gunners watahitaji kufanya vyema ikiwa wanataka kukipita kikosi cha Arne Slot.

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved