logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Usain Bolt aripotiwa kuibiwa mamilioni ya pesa kutoka kwa akaunti yake kwa ulaghai

Mwanariadha huyo alistaafu riadha miaka zaidi ya 6 iliyopita.

image
na Radio Jambo

Habari15 January 2023 - 07:44

Muhtasari


• Bolt ndio mshikilizi wa rekodi bora katika mbio za mita 100 na 200 ambazo aliweka miaka zaidi ya 10 iliyopita.

Usain Bolt anahofiwa kupoteza mamilioni ya pesa kwa ulaghai

Mwanariadha mshikilizi wa rekodi za dunia katika mbio za mita 100 na mita 200, Usain Bolt kutoka Jamaica anaripotiwa kupoteza mamilioni ya pesa kupitia ulaghai mkubwa.

Kulingana na jarida la AFP, mamlaka inayosimamia fedha nchini Jamaica imeanzisha uchunguzi dhidi ya kampuni ya kuwekeza pesa ambayo Bolt alikuwa amewekeza pesa zake na ambazo zimeofiwa kutoweka kwa njia za ulaghai.

Meneja wa Bolt Nugent Walker aliliambia gazeti la Jamaica Gleaner kwamba mwanariadha huyo aliyestaafu, mmoja wa wanariadha wakubwa wa wakati wote, amekuwa na uwekezaji na kampuni hiyo kwa zaidi ya muongo mmoja.

"Hatua zote muhimu zimechukuliwa ili kufafanua jambo hili," Walker aliambia jarida hilo, akisema mwanariadha huyo aligundua hitilafu na akaunti yake siku ya Jumatano.

"Amekuwa mteja wa kampuni hii kwa zaidi ya miaka 10...," aliongeza.

Gazeti hilo lilisema mamilioni ya dola yaliripotiwa kupotea kwenye akaunti ya Bolt.

Bolt alistaafu kutoka kwa riadha mnamo 2017 baada ya taaluma nzuri ambayo pamoja na medali nane za dhahabu za Olimpiki zilijumuisha medali 11 za dhahabu za Ubingwa wa Dunia.

 

Bolt alijizolea umaarufu duniani katika Michezo ya Olimpiki ya Beijing mwaka wa 2008 aliposhinda mbio za mita 100 na 200, akiweka rekodi mpya za dunia katika mbio zote mbili.

Mjamaika huyo aliendelea kushinda mbio zote mbili katika Michezo ya London ya 2012 na Rio 2016.

Miaka zaidi ya saba tangu kustaafu mbio, rekodi zake katika mita 100 na mita 200 bado zinasalia kama rekodi bora na hakujatokea mwanariadha mwingine wa kuzipiku.

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved