Bara la Afrika bado halina dhahabu siku 5 baada ya Olimpiki kuanza

Tunisia ndiyo timu ya pekee ya Afrka ambayo imebeba medali ya fedha

Muhtasari

•Tunisia ndiyo timu yenye ufanisi mkubwa zaidi kutoka Afrika kwa nafasi ya 16, ikiwa na medali ya fedha katika mashindano ya Fencing ya wanaume 

•Japani na Korea Kusini wanaongoza kwenye orodha ya medali zikiwa na medali 7 kila mmoja

walipigwa na Argentina na Australia.
Shujaa 7s walipigwa na Argentina na Australia. walipigwa na Argentina na Australia.
Image: HISANI

Nchi za Afrika zinapitia changamoto, kwani hakuna hata moja kati ya nchi 55 za bara hili iliyoshinda medali ya dhahabu katika Michezo ya Olimpiki ya awamu ya 33 huko Paris, Ufaransa, baada ya siku 5 za mashindano.

Tunisia ndiyo timu yenye ufanisi mkubwa zaidi kutoka Afrika kwa nafasi ya 16, ikiwa na medali ya fedha katika mashindano ya Fencing ya wanaume kupitia Ferjani Fares.

Misri wanafuata na medali ya shaba katika Fencing huku Afrika Kusini ikiwa imeshinda medali ya shaba katika Rugby Sevens kwa wanaume.

Wawakilishi wa Asia, Japani na Korea Kusini wanaongoza kwenye orodha ya medali zikiwa na medali 7 kila mmoja, ikiwa ni pamoja na dhahabu 4, fedha 2 na shaba 1, wakifuatwa na Australia yenye medali 6, dhahabu 4 na fedha 2.

Marekani ipo katika nafasi ya 4 kwa medali 12, ikiwa na dhahabu 3, fedha 6 na shaba 3, wakati wenyeji Ufaransa wanakamilisha nafasi ya 5 kwa medali 3 za dhahabu, fedha 3 na shaba 2.

Miongoni mwa mambo ya kushangaza na kuduwaza zaidi kwa bara la Afrika ni kwenye mchezo wa vikapu ambapo ushindi wa Sudan Kusini dhidi ya Puerto Rico kwa alama 90-79 katika mechi ya ufunguzi wa kundi C la mpira wa kikapu Jumapili, ikifanywa kuwa timu ya kwanza kutoka Afrika kushinda mechi ya Olimpiki.

Nchi nyingi za Afrika zinatarajiwa kuanza kushinda medali za dhahabu mara mashindano ya riadha yatakapoanza tarehe 1 Agosti.