logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Ramos atia saini mkataba wa miaka miwili na PSG

. PSG itakuwa timu yake ya tatu kuwakilisha

image
na Radio Jambo

Yanayojiri08 July 2021 - 10:27

Muhtasari


•Ramos ambaye mkataba wake na Real ulitamatika mwishoni mwa msimu wa 2020/21 ametia saini ya miaka miwili na mabingwa mara tisa wa kombe la ligue 1 nchini Ufaransa, Paris Saint-Germain.

Sergio Ramos

Baada ya kuichezea klabu ya Real Madrid kwa kipindi cha miaka 16, hatimaye mlinzi Sergio Ramos ataiwakilisha klabu nyingine msimu ujao.

Ramos ambaye mkataba wake na Real ulitamatika mwishoni mwa msimu wa 2020/21 ametia saini ya miaka miwili na mabingwa mara tisa wa kombe la ligue 1 nchini Ufaransa, Paris Saint-Germain.

Raia huyo wa Uhispania alicheza katika mechi 671 na Real Madrid na kufunga mabao 101. Ametajwa kama mmoja wa walinzi bora duniani huku akitajwa katika nafasi ya saba kwenye orodha ya tuzo la Ballon d'Or mwaka wa 2017.

Ramos ambaye ana umri wa miaka 35 alianza taaluma yake ya kucheza kandanda  mwaka wa 2003 na klabu ya Sevilla. PSG itakuwa timu yake ya tatu kuwakilisha.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved