logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mwanasoka wa Ufaransa, Jean-Pierre Adams, ambaye alikuwa amekosa fahamu kwa miaka 39 aaga dunia

Mlinzi huyo alipoteza fahamu akiwa na umri wa miaka 34 kufuatia kosa la 'anaesthesia' alipokuwa anapasuliwa goti kufuatia jeraha mnamo Machi 17, 1982

image
na Radio Jambo

Habari06 September 2021 - 10:41

Muhtasari


•Mzaliwa huyo wa Dakar, Senegal alipoteza fahamu akiwa na umri wa miaka 34 kufuatia kosa la 'anaesthesia' alipokuwa anapasuliwa goti kufuatia jeraha mnamo Machi 17, 1982.

Mwanasoka wa kitambo wa timu ya kitaifa ya Ufaransa  Jean-Pierre Adams, ambaye amekuwa kwenye  'coma' tangu mwaka wa 1982 ameaga dunia akiwa na umri wa miaka 73.

Kifo cha Adams kilithibitishwa asubuhi ya Jumatatu  katika hospitali ya chuo kikuu cha Nimes baada yake kukosa fahamu kwa kipindi cha miaka 39.

Mzaliwa huyo wa Dakar, Senegal alipoteza fahamu akiwa na umri wa miaka 34 kufuatia kosa la 'anaesthesia' alipokuwa anapasuliwa goti kufuatia jeraha mnamo Machi 17, 1982.

Kabla ya upasuaji uliomletea madhara yale kufanyiwa, mlinzi huyo ambaye alichezea Ufaransa kwenye mechi 22 aliripotiwa kuwa mzima na tayari kufanyiwa upasuaji.

Adams alipewa madawa ya kumfanya apoteze fahamu kwa kipindi cha masaa machache ili afanyiwe upasuaji bila kuhisi uchungu ila  hakuwahi amka baada ya upasuaji huo.

Kifo cha Adams kimethibitishwa na magazeti ya Ufaransa.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved