logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Everton yamtimua meneja wake Rafa Benitez

Ametimuliwa kufuatia msururu wa matokeo hafifu ambayo klabu hiyo imekuwa ikiandikisha hivi karibuni

image
na Radio Jambo

Makala17 January 2022 - 02:29

Muhtasari


•Ametimuliwa kufuatia msururu wa matokeo hafifu ambayo klabu hiyo imekuwa ikiandikisha hivi karibuni

Rafa Benitez

Klabu ya EPL ya Everton imesitisha mkataba wake na meneja wake Mhispania Rafael Benitez baada ya miezi saba tu.

Benitez ambaye alisajiliwa na Everton mwaka jana baada ya kuondoka kwa aliyekuwa meneja Carlo Ancelloti ametimuliwa kufuatia msururu wa matokeo hafifu ambayo klabu hiyo imekuwa ikiandikisha hivi karibuni.

Everton ilithibitisha kuondoka kwa Benitez siku ya Jumapili kupitia tovuti rasmi ya klabu huku ikitangaza kwamba mridhi wake atatafutwa hivi karibuni.

Hatua hii imejiri siku moja tu baada ya klabu hiyo kupoteza ugenini, 2-1 dhidi ya Norwich City  na kuongeza shinikizo kwa Benitez kutimuliwa.

Everton kwa sasa imekalia nafasi ya kumi na sita ikiwa na pointi 19 baada ya kuwa imeshiriki katika mechi 19 za EPL 2021/22.

Msimu uliopita klabu hiyo ilimaliza katika nafasi ya kumi ikijizolea pointi 59.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved