logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Algeria yabanduliwa nje ya AFCON kwa kichapo cha mabao 4-1

Algeria ambao ni mabingwa watetezi walibaduliwa kwenye hatua za makundi  kufuatia matokea mabaya waliyoandikisha  kwenye michuano hio.

image
na

Makala21 January 2022 - 04:57

Muhtasari


• Algeria imeyaaga rasmi mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika AFCON 2021 baada kupokezwa kichapo cha magoli 4-1 na timu ya Ivory Coast.

• Algeria ambao ni mabingwa watetezi wamebaduliwa kwenye hatua za makundi  kufuatia matokea mabaya waliyoandikisha  kwenye michuano hio

Nicolas Pepe akifunga bao la kwanza la Ivory coast

Timu ya Taifa ya Algeria imeyaaga rasmi mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika AFCON baada kupokea kichapo cha magoli 4-1 kutoka kwa timu ya Ivory Coast.

Algeria ambao ni mabingwa watetezi walibaduliwa kwenye hatua za makundi  kufuatia matokea mabaya waliyoandikisha  kwenye michuano hio.

Msururu wa Algeria kutopoteza mechi 35 ulitiwa doa wakati walinyukwa na Equatorial Guinea katika matokeo yalioacha wengi vinywa wazi. 

Mechi baina yao na Ivory Coast ilikuwa ya kutamatisha michuano ya makundi huku wakiwa na matumaini ya kufuzu kwa awamu ya maondoano.

Nicolas Pepe mchezaji wa Arsenal aliipa uongozi Ivory Coast, kipindi cha kwanza huku Frankie Kessie, Ibraham Sangare, na Sebastien Haller pia wakifunga bao moja moja mtawalia na kusaidia Ivory Coast kumaliza kileleni mwa kundi hilo kwa pointi saba.

Wakifuatwa na Equatorial Guinea kwa pointi sita. Algeria  walipewa penalti wakapoteza kupitia mchezaji anayecheza kabumbu ya kulipwa nchini Uingereza, Riyad Mahrez.

 

Mhariri: Davis Ojiambo


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved