logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Paul Pogba ajiunga tena na Juventus baada ya miaka 6

Pogba hakuwa ameichezea United tangu Aprili baada ya kusumbuliwa na jeraha.

image
na Radio Jambo

Makala11 July 2022 - 10:37

Muhtasari


•Pogba alisafiri kwa ndege hadi Turin siku ya Ijumaa kwa ajili ya vipimo vya matibabu kabla ya kutangazwa ramsi Jumatatu.

•United na Pogba hawakuweza kuafikiana kuhusu mkataba mpya na klabu hiyo ilithibitisha kwamba angeondoka kama mchezaji huru.

Paul Pogba amejiunga tena na Juventus kwa uhamisho wa bila malipo baada ya mkataba wake Manchester United kumalizika.

Kiungo huyo wa kati wa Ufaransa mwenye umri wa miaka 29 alishinda taji la Serie A mara mbili na miamba hao wa Italia kabla ya uhamisho wa rekodi ya dunia wa £89m kwenda United mwaka 2016.

Alisafiri kwa ndege hadi Turin siku ya Ijumaa kwa matibabu yake kabla ya kutangazwa ramsi Jumatatu.

Pogba hakuwa ameichezea United tangu Aprili baada ya kusumbuliwa na jeraha.

Juventusi alisema: "Tunapoagana baada ya tukio kubwa lililoshirikiwa pamoja, daima kuna matumaini kwamba tutaonana tena, mapema au baadaye.

"Aliondoka akiwa mvulana na anarudi kama mwanamume na bingwa, lakini kuna jambo moja ambalo halijabadilika - hamu ya kuandika kurasa zisizosahaulika za historia ya klabu kwa mara nyingine tena. Pogba amerejea na hatukuweza kuficha furaha."

United na Pogba hawakuweza kuafikiana kuhusu mkataba mpya na klabu hiyo ilithibitisha mwanzoni mwa Juni kwamba ataondoka kama mchezaji huru msimu huu wa joto.

Pogba alijiunga na akademi ya United kutoka Le Havre.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved