logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Fainali ya Kombe la Dunia: Messi 'anataka kuendelea' kuichezea Argentina

Messi atafikisha miaka 36 mwaka ujao lakini anaamini ana mengi ya kuipatia taifa lake.

image
na Radio Jambo

Habari19 December 2022 - 03:47

Muhtasari


•Lionel Messi anasema hatastaafu soka la kimataifa baada ya kuiongoza Argentina kunyakua kombe la dunia.

•"Aliongeza: "Ni wazi nilitaka kumaliza kazi yangu na hii na siwezi kuuliza chochote zaidi.

Lionel Messi anasema hatastaafu soka la kimataifa baada ya kuiongoza Argentina kunyakua kombe la dunia kwa mara ya kwanza katika kipindi cha miaka 36.

Mshambulizi huyo wa Paris St-Germain aliulizwa kuhusu mustakabali wake na kituo cha televisheni cha Argentina TyC Sports baada ya ya taifa hilo la Amerika Kusini kuilaza Ufaransa kwa mikwaju ya penalti 4-2 kufuatia sare ya 3-3.Messi atafikisha miaka 36 mwaka ujao lakini anaamini ana mengi ya kuipatia taifa lake.

"Ninapenda soka, ndivyo ninavyofanya," alisema.

"Ninafurahia kuwa katika timu ya taifa na ninataka kuendelea kwa kushuhudia michezo michache zaidi kama bingwa wa dunia.

"Aliongeza: "Ni wazi nilitaka kumaliza kazi yangu na hii na siwezi kuuliza chochote zaidi.

"Messi, akicheza Kombe lake la tano la Dunia, alifunga mara mbili kwenye fainali na pia alifunga penalti kwenye mikwaju ya penalti.Alishinda Mpira wa Dhahabu wa mashindano hayo - uliotunukiwa mchezaji bora - baada ya kufunga mabao saba.

Messi atakuwa na umri wa miaka 39 wakati wa Kombe lijalo la Dunia na alikuwa amedokeza hapo awali kwamba toleo hili nchini Qatar lingekuwa la mwisho kwake.

Hata hivyo, kocha Lionel Scaloni anasema anamtaka Messi katika kikosi chake kwa ajili ya michuano ya 2026, itakayofanyika Marekani, Canada na Mexico.

"Kwanza kabisa, tunahitaji kumwekea nafasi katika kikosi chate cha Kombe lijalo la Dunia 2026," alisema."Ikiwa anataka kuendelea kucheza, atakuwa nasi.

Nafikiri ana haki zaidi ya kuamua kama anataka kuendelea kuichezea Argentina au la, au anachotaka kufanya katika maisha yake ya soka."Ni furaha kubwa kwetu kumfundisha yeye na wachezaji wenzake.

"Kila kitu anachokutana nacho hadi wachezaji wenzake ni kitu kisicho na kifani, kitu ambacho sijawahi kuona. Mchezaji, mtu anayetoa sana kwa wenzake."


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved