logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Brighton wamfanya Mwepu, 24, kuwa kocha baada ya kustaafu kutokana na matatizo ya Moyo

Klabu ya Brightonc alikokuwa akicheza walimpa nafasi ya pili maishani kwa kumfanya kocha.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri31 December 2022 - 06:07

Muhtasari


• Mwepu sasa atakuwa anawanoa vijana wasiozidi umri wa miaka 9 katika akademia ya Brighton & Hoven.

Enock Mwepu, kiungo wa Brighton

Aliyekuwa kiungo wa Brighton Enock Mwepu na ambaye alilazimika kustaafu kucheza soka akiwa na umri wa miaka 24 tu kufuatia ugonjwa wa moyo hatimaye nyota yake imeng’aa tena.

Mwepu, raia wa Zambia mwenye umri wa miaka 24 alitangaza kustaafu miezi michache iliyopita baada ya kupatikana na matatizo ya moyo ambayo daktari walisema hangeweza tena kuendelea kukimbia uwanjani.

Klabu ya Brighton & Hoven ambayo alikuwa akichezea mpaka kupata taarifa hizo za kushtusha sasa imeripotiwa kumpa nafasi ya pili Mwepu kwa kumteua kuwa kocha wa vijana wasiozidi umri wa miaka 9 katika klabu hiyo ya Uingereza.

Alicheza muda mwingi wa uchezaji wake katika klabu ya RB Salzburg kabla ya kujiunga na timu ya Premier League kwenye dirisha la usajili la majira ya kiangazi mwaka 2021 kwa ada ya Euro milioni 23.

“Kwa kuwa hawezi kucheza soka tena, ameamua kwenda kufundisha na ameanza safari yake mpya kama kocha wa akademi ya Brighton's under 9's akiambatana na klabu iliyomleta kwenye Premier League,” Jarida la Vanguard liliripoti.

Aliitwa "kompyuta" kama jina la utani wakati wa utoto wake na wakati wa kucheza kwa sababu ya akili yake wakati akicheza mpira. Alikuwa Nahodha wa timu ya taifa ya Zambia ya "Chipolopolo boys" kabla ya kustaafu.

Baada ya habari hizo kuthibitishwa na klabu, Mwepu alitweet:

“Mpango wa Mungu na wakati wake daima ni kamilifu. Kumaliza mwaka kwa furaha. mimi ni wa Kristo Yesu.”

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved